FIKIRIA: Mwanamke, unamuacha mumeo (Mwanaume wako) kwasababu ya usaliti, alioufanya kuwa na mwanamke mwingine, (Aah!)
Mna familia pamoja, mtoto mmoja" au
wawili. (Ok!)
Hivyo, ukaomba talaka na mkatalikiana kwa sababu
umeumizwa sana na usaliti wake na huwezi kuuvumilia! Na baada ya mchakato wa
talaka kukamilika, ukaondoka na watoto wako! (Ooh!)
Ukaanza kufanya kazi kwa bidii ili ujipatie
mahitaji yako na uwalelee watoto wako mweyewe bila kuonyesha kuhitaji msaada wa
baba yao na kuzimudu gharama za maisha mwenyewe. (Good)
Ili kuendana na kuongezeka gharama za maisha,
unaangukia kwa mwanaume mwengine ‘Labda tajiri) Hujali chochote maana unahitaji
kulipa ada za watoto kama mwanamke unayejiamini na unajitegemea unahitaji
kuuthibitishia ulimwengu unajiweza mwenyewe kwa yote ndio maana ukakubali kuwa
na mwanaume huyo tajiri katika penzi la siri ingawa unafahamu ni mume wa mtu.
(Unajikuta umerudia kosa lilelile lililofanya nyie kutengana kwa talaka)
Hatimaye sasa na wewe umekua mchepuko kwa mume
wa mtu, tena mwenye familia yake na watoto pia (side chick to cheating
situation)
Ndipo unakumbuka na unaanza kufikiria kuhusu
mwanamke wa pembeni aliyekua naye mumeo, na kwa nini alikua naye! “Umechelewa’
Nda yako haipo tena!
Ulichofanya, ndicho alichokifanya mwanamke
uliyemfuma na mume wako, hukufikiria kuhusu maadili, na unaanza kumuelewa
taratibu: Pengine alikuwa na mume wako kwasababu ya ugumu wa maisha, wingi wa
majukumu, watoto aliotelekezewa wa kuwalea! Na zaidi tumbo linalohitaji chakula
kila siku.
NA SASA: Kama yule tu, unatamani hata kumpigia
mwanaume wa sasa uliye naye, lakini huwezi sababu unatambua yupo na mke wake na
familia yake nyumbani, na wewe unalinda nafasi yako kwake maana mkewe akigundua
hawezi kukimbilia kuachana zaidi wewe ndio utaachika. “Mateso yanarudia tena
upya”
Hivyo amekupa masharti yake ambayo utake
usitake lazima uyafuate, na unapaswa kuheshimu faragha yao kuwa sasa yupo
nyumbani na familia yake na wewe utaendelea kuwa option-tu, Linapokuja swala la
Kupunguza mawazo na tamaa zake.
Unafikiria tu kuhusu maumivu yako!
Unafikiria tu kuhusu faraja (Consolation) yako!
Ila walau awali ulikuwa na mume wako pekee
yako’ Ndio alikusaliti lakini bado aliendelea kuwa wako!
Hatimaye unajaribu kutafuta tena kufahamu juu
ya yanayoendelea kwenye maisha yake baada ya kutalikiana na kila mmoja kushika
maisha yake, unang’amua sasa ame ‘move-on’, na tayari anaishi na mwanamke
mwingine pengine mdogo kiumri au mrembo kukuliko wewe.
Unakaza roho, kwakua mawasiliano yake bado
unayo unaamua kupigia na kumuomba miadi ya kukutana sehemu kuongea kwa kigezo
cha watoto wame-mmisi wanataka aje kuwatembelea, kweli anafika na kuwaletea
vizawadi watoto na kukuachia pesa kidogo ya matumizi ya watoto, lakini
haitoshelezi kama ilivyokuwa zamani. (Mke mpya ameshikilia matumizi yake yote)
Mnapanga kutoka matembezi kidogo,
mnakumbushiana wakati mzuri mliokuwa nao zamani na hamadi-bila kutarajia, na
ngono mnashiriki! Kwa muda mchache unasahau taabu na dhiki na upweke uliokuwa
nao wote!
Punde, mmemaliza kila kitu anakuaga kurudi kwa
mkewe anapiga simu, ghafla unagundua sio wako tena na dhiki, taabu na upweke
unarudi kama ulivyokuwa siku zote!
NDIPO: Unagundua sasa unahusiana ‘dating’ na
wanaume wawili tofauti, ambapo wote wawili wamewasaliti wake zao na wewe ndio
sababu!
Ghafla unaikumbuka ndoa yako, uhuru uliokuwa
nao ukiwa na mume wako wa ndoa, kisha unagundua ni kama dunia nzima imekugeukia
na maisha hayako sawa kwako!
Unaweza kudhani hii ni stori tu, lakini kuna
wanawake wanaoiishi kiuhalisia, na ninge’ au ningalijua huja baada ya kuwa
tukio lishatokea. Siungi usaliti ndoani, Lakini pia siungi vitendo vya ukatili ndoani" Mninukuu vizuri!
Mbali ya tofauti zetu, familia ni baba na mama na sio mzazi mmoja, licha ya changamoto zilizoko ndani ya familia hizo.
Asilimia kubwa ya ndoa zinawaka moto, na sio
salama kwa asilimia mia, (Ni kusameheana na kuvumiliana) Tafakari chukua hatua!
#MwalimuMeena (0778291375) Kwa Maoni, au Unahitaji ushauri wa ndoa nipo hapa kukushauri!
Unaweza
kusambaza elimu hii: (Share) iwafikie wengi zaidi, lakini (usi-copy na ku-paste)
na kufanya kama ni chanzo cha mawazo na Sanaa yako) ukifanya hivyo nipe credit
yangu katika chapisho lako. Asante!



No comments:
Post a Comment