Na.
Stewart Meena
Kutana na ndege wasio na sauti au
"mlio", wenye miguu mirefu na wenye kuweza kuhimili ongezeko kali la
joto" ikilinganishwa na ndege wengine warukao, na hiyo ikampatia sifa ya
upekee na majina mbalimbali kama:
"Undertaker, na Marabou storks" Kiswahili
wakijulikana kama ‘KORONGO MARABOU’
Ndege hawa, ni waviziaji na vyakula vyao vikuu
ni pamoja na mabaki ya mizoga ya wanyama tofauti, mabaki ya vyakula vitumiwavyo
na wanadamu, samaki pamoja na vyakula vingine kama, mijusi, nyoka, vyura,
wadudu, panya na ndege wengine wadogowadogo.
Makazi makuu ya ndege hawa ni maeneo yote
karibu na mito, maziwa, milimani ndani ya miamba, na kwenye hifadhi za
wanyamapori, tambarare zilizo na miti mirefu, ambapo licha ya urefu na ukubwa
wao, wanaweza kuruka katika eneo kubwa la anga na kupaa umbali mrefu.
Kuruka kwao, huweza kuruka hewani umbali wa
futi-13,000 (feet) toka usawa wa bahari, na inapokuja swala la mwendokasi
katika jamii yao ya ndege, Korongo huwenda hawa wakawa wana kiwango kidogo cha
mwendokasi huo.
UKWELI USIOUJUA KUHUSU NDEGE HAWA.
Marabou stork, ni miongoni mwa ndege wasiovutia (ugliest bird on the world) kwa kuwatazama, kwa mwonekano wao (wakiwa na Miguu mirefu, shingo ndefu na eneo kama tumbo la kuhifadhia chakula linaloning’inia karibu na shingo yao likiwa na rangi ya pinki (Eng: a pink gular sac).
Ndege korongo huyu, hutambulikana pia kama
ndege muuwaji kwa muonekano wake kwa nyuma ukiwa unamtazama, wazungu wakimuita “Nature’s
eyesore / the undertaker bird” na ndiye ndege jamii ya tai mwenye miguu mirefu
katika jamii hiyo centimita karibu 50, huku mbawazao zikiwa na urefu wa futi11
na kuwafanya ndege hawa kuwa na upekee tofauti na ndege wengine.
Sambamba na ndege wote kuwa au kutambulikana
pia kwa milio yao, ndege hawa hawana milio hiyo, ingawa huweza kuwasikia
wakitoa milio Fulani inayotokana na kugongesha midomo yao au mbawa zao.
Hadi kufikia umri wa ukomavu ndege hawa,
huchukua karibu miaka mine ‘4’ na kuwafanya miongoni mwa ndegw wanaokua
taratibu-taratibu Zaidi ikilinganishwa na ndege wengine wanapoanguliwa kwenye
mayai yao.
Korongo hawa wa marabou, hupatikana pekee yake
barani Afrika (Ukiacha waliohifadhiwa katika zoo za wanyama) kwenye maeneo ya
kitropiki kwenye nchi kama, Senegal, Eritrea, Ethiopia, Somalia, Tanzania,
Kenya, Uganda, Namibia, Congo, Afrika ya Kusini nk.
(Unaweza kusoma pia hapa)
Kwa nchi ya Tanzania: Ndege hawa ni maarufu Zaidi
kwenye ukaanda wa ziwa Victoria na Tanganyika, na huweza kuwaona Zaidi kwenye
hifadhi ya taifa ya Serengeti, Manyara, Nyerere, Tarangire nk. Ambapo wenyeji
wa mikoa ya Manyara, Mara, Mwanza, Geita ndege hawa huingia hadi maeneo ya
masoko na mijini.
Marabou (Korongo) ni ndege anayependa
kuchangamana Zaidi na binadamu ndani ya makazi yao na hii ni kwa ajili ya
urahisi wa kupata vitoweo vyao, huku wale kwenye hifadhi ya wanayama hupendelea
Zaidi kuwa karibu na wanyama wawindaji kama Fisi, Chui, Duma, Simba na Mbweha
ikiwa ni sehemu rahisi kwao kuvizia mawindo yao na kuyaiba. (Marabou stork are
known to be scavenger bird) Kimsingi ndege hawa korongo sio wawindaji hodari,
ila ni waviziaji hodari.
Picha: Natalie Carberi
Wanawezaje Kuhimili Joto Kali La Uwanda Wa
Savana?
Ili kupunguza ongezeko la joto na jua kali
linalowatesa ndege wengi, kwa ndege Korongo ni tofauti kidogo, ambapo miili yao
inauwezo wa asili wa kubadili kanijoto mwili wao kuendana na ukali wa jua au
joto la maeneo waliyopo, kuficha uso wao ndani ya mabawa na kutanua mfuko wao
wa pinki uliopo chini ya shingo huwawezesha kuendana na mabadiliko hayo ya
joto.
Na endapo kutakua na baridi kali na wanahitaji
joto, basi hutanua mabawa yao (mbawa) na hiyo huwawezesha kurudisha kwa haraka
ongezeko lao hilo la joto ndani ya miili yao.
Kimazingira kwenye jamii yao, huwenda hawa
ndio ndege wavivu zaidi na wasiopenda kuhangaika kutafuta vitoweo, isipokua
kusimama karibu na wanaotafuta (kuwinda) na wakishapata kitoweo chao wao ndio
huenda eneo hilo na kuwafurusha kwa ajili ya kuiba kitoweo hicho. Mfano: Kanda
ya ziwa huiba samaki zilizovuliwa na wavuvi.
Mazaliano yao hupendelea zaidi majira ja
kiangazi wakati kina cha maji maeneo mengi yakiwa yameshuka au kukauka, kwani
ndio urahisi zaidi wa wao kupata vitoweo vyao kwa urahisi zaidi.
Ni msimu huu huweza kuwaona ndege hawa wakiwa
karibu-karibu zaidi, na madume wakipambana kwa midomo yao ili kuwania haki ya
kumiliki korogo jike kwa ajili ya mwanzo wa mazalia yao, ambapo atakayeshinda
ndio kuanzia hapo ataambatana na jike husika kwa muda wote wa kujenga kiota,
kurutubisha mayai, kutaga na kuyaatamia, kisha watoto watakao anguliwa
kushirikiana kuwatafutia chakula kwa pamoja hadi watakapoweza kujitegemea
wenyewe.
Ndege hawa wakishaungana, huishi hivyo wawili
pekee kifamilia hadi mwisho wa maisha yao, na ajabu nyingine ni kuwa
hawachanganyi mwenza na ikitokea mmoja kati yao amekufa mwingine huakia hivyo
hivyo na huelezwa, sababu ya upweke na yeye hachukui muda mrefu kabla ya kufa, ambapo
baadhi ya tafiti husema ndege mwenza aliyesalia huweza kujinyima chakula kama
njia ya yeye kufa.
Waweza pia kusoma HAPA
MWISHO: Kwa sababu ya urefu wa miguu yao, mbawa zao na midomo yao hii huwafanya kuwa na uwiano sawa wenye kupungua uzito hivyo kumuwezesha kuruka kwa urahisi zaidi wanapopaa angani, ikilinganishwa na jamii nyingine za ndege walio na urefu na uzito kama wa kwake.
Pia eneo la pinki karibu na shingo yake,
hutumia hapo kama akiba ya kuhifadhi chakula chake akiwa ameshiba, kisha kula kwa
wakati mwingine hususani anapokuwa ana njaa.
Tafadhali unaposasisha (Kushare taarifa hii),
hakikisha unatambulisha chanzo cha taarifa hii kwa kutupa ‘credit’ Asante! StewartMeena

No comments:
Post a Comment