
Picha: JohnsHopkin Health Blog
Kuingia hedhi ni jambo la kawaida kwa kila binti/msichana aliyepevuka itoshe kusema "Ni jambo la kujivunia" kwakuwa hedhi ni kipimo sahihi cha kuwa Mwanamke ambaye siku za usoni utatarajia kuitwa mama; na ikiwa binti huioni hedhi yako inapaswa kuwaona madaktari mapema kutibu na kushughulikia tatizo hilo haswa kwa wasichana waliokatika umri wa kuvunja ungo (kupevuka)
Nini hutokea wakati wa hedhi!?: Kibiolojia hedhi hutokea baada ya kupita zile siku za urutubishaji wa yai (Ovulation circle) ambapo hii hutukia wiki ya3 kwa wanawake wengi wenye mzunguko wa siku21, 28 na 31.
Wakati huu, Yai ambalo halijarutubishwa (kwa kukutana na mwanaume) hutolewa kutoka kwenye ovari za mwanamke kwa mfumo maalimu wa mwili (kuflashi) na hapo muhusika huweza kuona uchafuuchafu wa kawaida, na damu kwa muda wa siku2, 3 au 4, huku wengine wakienda mpaka wiki moja (siku7) ambapo hii watabibu wengi huieleza kuwa sio nzuri sana kiafya, ila kikawaida inatakiwa siku4 iwe imekata.
Ni wakati huu wa hedhi: Wanawake wengi hupitia madhila mbalimbali yakiambatana na #maumivu_makali chini ya kitovu, kuumwa na kiuno na mgongo, kichefuchefu, kukosa hamu ya kula na kutapika.
Nikiwanukuu baadhi ya kina dada wanasema:
"Mimi staki kuongea maana nahesabu siku tu nianze kuhangaika daa mungu sijui sababu zake lakini kwakweli ata ukielezea akuna atakaye kuamini";
- "Tunywe Maji Ya Karafuu, Ikifika Siku Wala Tumbo Haliumi"
- "Chai ya moto yenye mchanganyiko wa tangawizi, karafuu, mdalasini, hiliki inanisaidia sana"
- "Ikianza tuu day one chemsha mizizi ya mkunde pori kunywa ila hii #kupata_mimba ni nje nje inasaidia na tatizo halijirudii me nshasahau hzo mambo za kuumwa tumbo baada ya kupata ujauzito na kujifungua"
- "Kpindi Cha ubinti wangu nilikuwa naumwa mnoo yaani hadi home walikuwa wanajua, lakini tangu nijifungue mwanangu siumwi tena na chochote yaan"
- "Tumbo la P, mdogo wangu alikuwa anaumwa mpaka anazimia... Ila tulijitajidi kumchemshia #mzugwa mara nyingi tuwezavyo sa hivi anaumwa ila cyo km zamani"
Asante kwa kutufuatilia, na tafadhali Like page hii: https://www.facebook.com/stewart.meena na utu - Follow, ili kusoma na kupata habari, na makala nyinginezo za kuvutia kama hizi.
No comments:
Post a Comment