Sunday, 30 August 2026
MJI MTAKATIFU WA JERUSALEM, MWINGILIANO, CHANZO IMANI ZA DINI TOFAUTI
Thursday, 27 August 2026
MWANAMKE: KWANINI TALAKA HAIPASWI KUWA SULUHISHO LA MGOGORO JUU YA USALITI!
FIKIRIA: Mwanamke, unamuacha mumeo (Mwanaume wako) kwasababu ya usaliti, alioufanya kuwa na mwanamke mwingine, (Aah!)
Mna familia pamoja, mtoto mmoja" au
wawili. (Ok!)
Hivyo, ukaomba talaka na mkatalikiana kwa sababu
umeumizwa sana na usaliti wake na huwezi kuuvumilia! Na baada ya mchakato wa
talaka kukamilika, ukaondoka na watoto wako! (Ooh!)
Ukaanza kufanya kazi kwa bidii ili ujipatie
mahitaji yako na uwalelee watoto wako mweyewe bila kuonyesha kuhitaji msaada wa
baba yao na kuzimudu gharama za maisha mwenyewe. (Good)
Ili kuendana na kuongezeka gharama za maisha,
unaangukia kwa mwanaume mwengine ‘Labda tajiri) Hujali chochote maana unahitaji
kulipa ada za watoto kama mwanamke unayejiamini na unajitegemea unahitaji
kuuthibitishia ulimwengu unajiweza mwenyewe kwa yote ndio maana ukakubali kuwa
na mwanaume huyo tajiri katika penzi la siri ingawa unafahamu ni mume wa mtu.
(Unajikuta umerudia kosa lilelile lililofanya nyie kutengana kwa talaka)
Hatimaye sasa na wewe umekua mchepuko kwa mume
wa mtu, tena mwenye familia yake na watoto pia (side chick to cheating
situation)
Ndipo unakumbuka na unaanza kufikiria kuhusu
mwanamke wa pembeni aliyekua naye mumeo, na kwa nini alikua naye! “Umechelewa’
Nda yako haipo tena!
Ulichofanya, ndicho alichokifanya mwanamke
uliyemfuma na mume wako, hukufikiria kuhusu maadili, na unaanza kumuelewa
taratibu: Pengine alikuwa na mume wako kwasababu ya ugumu wa maisha, wingi wa
majukumu, watoto aliotelekezewa wa kuwalea! Na zaidi tumbo linalohitaji chakula
kila siku.
NA SASA: Kama yule tu, unatamani hata kumpigia
mwanaume wa sasa uliye naye, lakini huwezi sababu unatambua yupo na mke wake na
familia yake nyumbani, na wewe unalinda nafasi yako kwake maana mkewe akigundua
hawezi kukimbilia kuachana zaidi wewe ndio utaachika. “Mateso yanarudia tena
upya”
Hivyo amekupa masharti yake ambayo utake
usitake lazima uyafuate, na unapaswa kuheshimu faragha yao kuwa sasa yupo
nyumbani na familia yake na wewe utaendelea kuwa option-tu, Linapokuja swala la
Kupunguza mawazo na tamaa zake.
Unafikiria tu kuhusu maumivu yako!
Unafikiria tu kuhusu faraja (Consolation) yako!
Ila walau awali ulikuwa na mume wako pekee
yako’ Ndio alikusaliti lakini bado aliendelea kuwa wako!
Hatimaye unajaribu kutafuta tena kufahamu juu
ya yanayoendelea kwenye maisha yake baada ya kutalikiana na kila mmoja kushika
maisha yake, unang’amua sasa ame ‘move-on’, na tayari anaishi na mwanamke
mwingine pengine mdogo kiumri au mrembo kukuliko wewe.
Unakaza roho, kwakua mawasiliano yake bado
unayo unaamua kupigia na kumuomba miadi ya kukutana sehemu kuongea kwa kigezo
cha watoto wame-mmisi wanataka aje kuwatembelea, kweli anafika na kuwaletea
vizawadi watoto na kukuachia pesa kidogo ya matumizi ya watoto, lakini
haitoshelezi kama ilivyokuwa zamani. (Mke mpya ameshikilia matumizi yake yote)
Mnapanga kutoka matembezi kidogo,
mnakumbushiana wakati mzuri mliokuwa nao zamani na hamadi-bila kutarajia, na
ngono mnashiriki! Kwa muda mchache unasahau taabu na dhiki na upweke uliokuwa
nao wote!
Punde, mmemaliza kila kitu anakuaga kurudi kwa
mkewe anapiga simu, ghafla unagundua sio wako tena na dhiki, taabu na upweke
unarudi kama ulivyokuwa siku zote!
NDIPO: Unagundua sasa unahusiana ‘dating’ na
wanaume wawili tofauti, ambapo wote wawili wamewasaliti wake zao na wewe ndio
sababu!
Ghafla unaikumbuka ndoa yako, uhuru uliokuwa
nao ukiwa na mume wako wa ndoa, kisha unagundua ni kama dunia nzima imekugeukia
na maisha hayako sawa kwako!
Unaweza kudhani hii ni stori tu, lakini kuna
wanawake wanaoiishi kiuhalisia, na ninge’ au ningalijua huja baada ya kuwa
tukio lishatokea. Siungi usaliti ndoani, Lakini pia siungi vitendo vya ukatili ndoani" Mninukuu vizuri!
Mbali ya tofauti zetu, familia ni baba na mama na sio mzazi mmoja, licha ya changamoto zilizoko ndani ya familia hizo.
Asilimia kubwa ya ndoa zinawaka moto, na sio
salama kwa asilimia mia, (Ni kusameheana na kuvumiliana) Tafakari chukua hatua!
#MwalimuMeena (0778291375) Kwa Maoni, au Unahitaji ushauri wa ndoa nipo hapa kukushauri!
Unaweza
kusambaza elimu hii: (Share) iwafikie wengi zaidi, lakini (usi-copy na ku-paste)
na kufanya kama ni chanzo cha mawazo na Sanaa yako) ukifanya hivyo nipe credit
yangu katika chapisho lako. Asante!
Monday, 24 August 2026
NINI HUTOKEA, MAUMIVU TUMBO LA HEDHI KWA WANAWAKE?

Picha: JohnsHopkin Health Blog
Kuingia hedhi ni jambo la kawaida kwa kila binti/msichana aliyepevuka itoshe kusema "Ni jambo la kujivunia" kwakuwa hedhi ni kipimo sahihi cha kuwa Mwanamke ambaye siku za usoni utatarajia kuitwa mama; na ikiwa binti huioni hedhi yako inapaswa kuwaona madaktari mapema kutibu na kushughulikia tatizo hilo haswa kwa wasichana waliokatika umri wa kuvunja ungo (kupevuka)
Nini hutokea wakati wa hedhi!?: Kibiolojia hedhi hutokea baada ya kupita zile siku za urutubishaji wa yai (Ovulation circle) ambapo hii hutukia wiki ya3 kwa wanawake wengi wenye mzunguko wa siku21, 28 na 31.
Wakati huu, Yai ambalo halijarutubishwa (kwa kukutana na mwanaume) hutolewa kutoka kwenye ovari za mwanamke kwa mfumo maalimu wa mwili (kuflashi) na hapo muhusika huweza kuona uchafuuchafu wa kawaida, na damu kwa muda wa siku2, 3 au 4, huku wengine wakienda mpaka wiki moja (siku7) ambapo hii watabibu wengi huieleza kuwa sio nzuri sana kiafya, ila kikawaida inatakiwa siku4 iwe imekata.
Ni wakati huu wa hedhi: Wanawake wengi hupitia madhila mbalimbali yakiambatana na #maumivu_makali chini ya kitovu, kuumwa na kiuno na mgongo, kichefuchefu, kukosa hamu ya kula na kutapika.
Nikiwanukuu baadhi ya kina dada wanasema:
"Mimi staki kuongea maana nahesabu siku tu nianze kuhangaika daa mungu sijui sababu zake lakini kwakweli ata ukielezea akuna atakaye kuamini";
- "Tunywe Maji Ya Karafuu, Ikifika Siku Wala Tumbo Haliumi"
- "Chai ya moto yenye mchanganyiko wa tangawizi, karafuu, mdalasini, hiliki inanisaidia sana"
- "Ikianza tuu day one chemsha mizizi ya mkunde pori kunywa ila hii #kupata_mimba ni nje nje inasaidia na tatizo halijirudii me nshasahau hzo mambo za kuumwa tumbo baada ya kupata ujauzito na kujifungua"
- "Kpindi Cha ubinti wangu nilikuwa naumwa mnoo yaani hadi home walikuwa wanajua, lakini tangu nijifungue mwanangu siumwi tena na chochote yaan"
- "Tumbo la P, mdogo wangu alikuwa anaumwa mpaka anazimia... Ila tulijitajidi kumchemshia #mzugwa mara nyingi tuwezavyo sa hivi anaumwa ila cyo km zamani"
Asante kwa kutufuatilia, na tafadhali Like page hii: https://www.facebook.com/stewart.meena na utu - Follow, ili kusoma na kupata habari, na makala nyinginezo za kuvutia kama hizi.Saturday, 22 August 2026
MFAHAMU NDEGE KORONGO AINA YA MARABOU, 'THE UNDERTAKER'
Na.
Stewart Meena
Kutana na ndege wasio na sauti au
"mlio", wenye miguu mirefu na wenye kuweza kuhimili ongezeko kali la
joto" ikilinganishwa na ndege wengine warukao, na hiyo ikampatia sifa ya
upekee na majina mbalimbali kama:
"Undertaker, na Marabou storks" Kiswahili
wakijulikana kama ‘KORONGO MARABOU’
Ndege hawa, ni waviziaji na vyakula vyao vikuu
ni pamoja na mabaki ya mizoga ya wanyama tofauti, mabaki ya vyakula vitumiwavyo
na wanadamu, samaki pamoja na vyakula vingine kama, mijusi, nyoka, vyura,
wadudu, panya na ndege wengine wadogowadogo.
Makazi makuu ya ndege hawa ni maeneo yote
karibu na mito, maziwa, milimani ndani ya miamba, na kwenye hifadhi za
wanyamapori, tambarare zilizo na miti mirefu, ambapo licha ya urefu na ukubwa
wao, wanaweza kuruka katika eneo kubwa la anga na kupaa umbali mrefu.
Kuruka kwao, huweza kuruka hewani umbali wa
futi-13,000 (feet) toka usawa wa bahari, na inapokuja swala la mwendokasi
katika jamii yao ya ndege, Korongo huwenda hawa wakawa wana kiwango kidogo cha
mwendokasi huo.
UKWELI USIOUJUA KUHUSU NDEGE HAWA.
Marabou stork, ni miongoni mwa ndege wasiovutia (ugliest bird on the world) kwa kuwatazama, kwa mwonekano wao (wakiwa na Miguu mirefu, shingo ndefu na eneo kama tumbo la kuhifadhia chakula linaloning’inia karibu na shingo yao likiwa na rangi ya pinki (Eng: a pink gular sac).
Ndege korongo huyu, hutambulikana pia kama
ndege muuwaji kwa muonekano wake kwa nyuma ukiwa unamtazama, wazungu wakimuita “Nature’s
eyesore / the undertaker bird” na ndiye ndege jamii ya tai mwenye miguu mirefu
katika jamii hiyo centimita karibu 50, huku mbawazao zikiwa na urefu wa futi11
na kuwafanya ndege hawa kuwa na upekee tofauti na ndege wengine.
Sambamba na ndege wote kuwa au kutambulikana
pia kwa milio yao, ndege hawa hawana milio hiyo, ingawa huweza kuwasikia
wakitoa milio Fulani inayotokana na kugongesha midomo yao au mbawa zao.
Hadi kufikia umri wa ukomavu ndege hawa,
huchukua karibu miaka mine ‘4’ na kuwafanya miongoni mwa ndegw wanaokua
taratibu-taratibu Zaidi ikilinganishwa na ndege wengine wanapoanguliwa kwenye
mayai yao.
Korongo hawa wa marabou, hupatikana pekee yake
barani Afrika (Ukiacha waliohifadhiwa katika zoo za wanyama) kwenye maeneo ya
kitropiki kwenye nchi kama, Senegal, Eritrea, Ethiopia, Somalia, Tanzania,
Kenya, Uganda, Namibia, Congo, Afrika ya Kusini nk.
(Unaweza kusoma pia hapa)
Kwa nchi ya Tanzania: Ndege hawa ni maarufu Zaidi
kwenye ukaanda wa ziwa Victoria na Tanganyika, na huweza kuwaona Zaidi kwenye
hifadhi ya taifa ya Serengeti, Manyara, Nyerere, Tarangire nk. Ambapo wenyeji
wa mikoa ya Manyara, Mara, Mwanza, Geita ndege hawa huingia hadi maeneo ya
masoko na mijini.
Marabou (Korongo) ni ndege anayependa
kuchangamana Zaidi na binadamu ndani ya makazi yao na hii ni kwa ajili ya
urahisi wa kupata vitoweo vyao, huku wale kwenye hifadhi ya wanayama hupendelea
Zaidi kuwa karibu na wanyama wawindaji kama Fisi, Chui, Duma, Simba na Mbweha
ikiwa ni sehemu rahisi kwao kuvizia mawindo yao na kuyaiba. (Marabou stork are
known to be scavenger bird) Kimsingi ndege hawa korongo sio wawindaji hodari,
ila ni waviziaji hodari.
Picha: Natalie Carberi
Wanawezaje Kuhimili Joto Kali La Uwanda Wa
Savana?
Ili kupunguza ongezeko la joto na jua kali
linalowatesa ndege wengi, kwa ndege Korongo ni tofauti kidogo, ambapo miili yao
inauwezo wa asili wa kubadili kanijoto mwili wao kuendana na ukali wa jua au
joto la maeneo waliyopo, kuficha uso wao ndani ya mabawa na kutanua mfuko wao
wa pinki uliopo chini ya shingo huwawezesha kuendana na mabadiliko hayo ya
joto.
Na endapo kutakua na baridi kali na wanahitaji
joto, basi hutanua mabawa yao (mbawa) na hiyo huwawezesha kurudisha kwa haraka
ongezeko lao hilo la joto ndani ya miili yao.
Kimazingira kwenye jamii yao, huwenda hawa
ndio ndege wavivu zaidi na wasiopenda kuhangaika kutafuta vitoweo, isipokua
kusimama karibu na wanaotafuta (kuwinda) na wakishapata kitoweo chao wao ndio
huenda eneo hilo na kuwafurusha kwa ajili ya kuiba kitoweo hicho. Mfano: Kanda
ya ziwa huiba samaki zilizovuliwa na wavuvi.
Mazaliano yao hupendelea zaidi majira ja
kiangazi wakati kina cha maji maeneo mengi yakiwa yameshuka au kukauka, kwani
ndio urahisi zaidi wa wao kupata vitoweo vyao kwa urahisi zaidi.
Ni msimu huu huweza kuwaona ndege hawa wakiwa
karibu-karibu zaidi, na madume wakipambana kwa midomo yao ili kuwania haki ya
kumiliki korogo jike kwa ajili ya mwanzo wa mazalia yao, ambapo atakayeshinda
ndio kuanzia hapo ataambatana na jike husika kwa muda wote wa kujenga kiota,
kurutubisha mayai, kutaga na kuyaatamia, kisha watoto watakao anguliwa
kushirikiana kuwatafutia chakula kwa pamoja hadi watakapoweza kujitegemea
wenyewe.
Ndege hawa wakishaungana, huishi hivyo wawili
pekee kifamilia hadi mwisho wa maisha yao, na ajabu nyingine ni kuwa
hawachanganyi mwenza na ikitokea mmoja kati yao amekufa mwingine huakia hivyo
hivyo na huelezwa, sababu ya upweke na yeye hachukui muda mrefu kabla ya kufa, ambapo
baadhi ya tafiti husema ndege mwenza aliyesalia huweza kujinyima chakula kama
njia ya yeye kufa.
Waweza pia kusoma HAPA
MWISHO: Kwa sababu ya urefu wa miguu yao, mbawa zao na midomo yao hii huwafanya kuwa na uwiano sawa wenye kupungua uzito hivyo kumuwezesha kuruka kwa urahisi zaidi wanapopaa angani, ikilinganishwa na jamii nyingine za ndege walio na urefu na uzito kama wa kwake.
Pia eneo la pinki karibu na shingo yake,
hutumia hapo kama akiba ya kuhifadhi chakula chake akiwa ameshiba, kisha kula kwa
wakati mwingine hususani anapokuwa ana njaa.
Tafadhali unaposasisha (Kushare taarifa hii),
hakikisha unatambulisha chanzo cha taarifa hii kwa kutupa ‘credit’ Asante! StewartMeena
Wednesday, 19 August 2026
ATHARI / MADHARA YA KUKAA NA HAJA NDOGO KWA MUDA MREFU
![]() |
| Image by: Harbin Clinic |
Utakubaliana na mimi kwamba, kitendo cha mtu kubanwa na haja ndogo siyo kitu cha hiyari kwamba sasa mtu anaamua ngoja nibanwe na mkojo, hili ni jambo la asili na ni matokeo ya vyakula, matunda au vinywaji tunavyotumia. Kwa lugha nyingine tumekuwa tukiita kuwa ni wito wa asili au nature’s call.
Yawezekana mtu akawa katika mkutano, safarini, akawa katika
mitandao ya kijamii anachati au popote pale akiwa anafanya jambo fulani na
kutokana na jambo hilo, mtu akaendelea kujibana na kutokwenda kuyapunguza maji-taka mwili, haya kutoka katika kibofu cha mkojo kwa kutoa kipaumbele kwa shughuli
anayoifanya kuliko kusikiliza kwanza wito huu wa asili 'kuwa kibofu chake kimejaa.
Mambo haya tunayafanya sana, utasikia, mkojo umenibana kweli,
ila ngoja nimalizie hii kazi halafu niende kujisaidia, hivi ndivyo watu wengi
wafanyavyo kimazoea kitu ambacho hakishauriwi kitabibu na kwa afya ya mwili wako.
Kutokana na vyakula na vinywaji tunavyotumia katika milo yetu kila wakati, kibofu cha mkojo
huanza kujaa mkojo, unaojitengeneza wakati vyakula vinachaguliwa (Kuchakatwa) na mwili, hivyo mkojo unapofikia karibu mililita 50 mpaka 500 mtu huyo husika huanza
kuhisi hitaji la kwenda haja ndogo (kukojoa).
Kibofu cha mkojo kimezungukwa na vigunduzi asili (Receptors)
vinavyopeleka taarifa katika Ubongo kuonyesha kuwa kibofu cha mkojo kimekaribia
au kimejaa, baada ya taarifa hizi kufika katika ubongo, ubongo unatoa taarifa
katika kibofu cha mkojo ili kiweze kushikilia mkojo huo kwa kuikaza misuli
maalumu (Sphincters) mpaka hapo muda wa wewe kwenda kukojoa utakapofika.
Kibofu cha mkojo hufanya kazi kwa mfumo wa kujiendesha wenyewe
yaani, automatic, kitendo cha mtu kupuuzia kwenda kukojoa husababisha Ubongo
upate usumbufu wa taarifa za kujaa kwa kibofu cha mkojo na kwa kuwa Ubongo nao
hutuma taarifa katika kibofu cha mkojo kusema kuwa mkojo uendelee kushikiliwa
mpaka muda muafaka utakapofika, itafika kipindi uwezo wa ubongo kutoa taarifa
hizi na pia uwezo wa vigunduzi asili (Receptors) vilivyoko katika kibofu cha
mkojo kupoteza uwezo wake tena wa kufanya kazi hizo au uwezo kuwa mdogo.
Matokeo yake ni mtu siku kweli anahitajika kuvumilia kidogo ili
afike sehemu inayostahihi kujisaidia, lakini hawezi tena na kujikuta muda mdogo
tu….mtu tayari kaloanisha nguo yake.
Mpenzi msomaji, mtu kujibana na kupuuzia kwenda haja ndogo mara
kwa mara husababisha uwezo wa kibofu chake cha mkojo kushindwa kujitawala upotee.
Pia kama uwezo wa neva zinazopeleka taarifa kwenye ubongo kuhusu
mabadiliko/ujazo wa kibofu cha mkojo zitaharibika, basi misuli maalumu ya
kubana mkojo (sphincter) itashindwa kuachia na matokeo yake mtu ataendelea
kukaa na mkojo katika kibofu chake kwa muda mwingi zaidi kitu ambacho ni hatari
kwa afya yake.
Endapo mkojo huu utashindwa kutoka, utatengeneza mazalia ya
bakteria na kukusababishia magonjwa ya kibofu (bladder infection), kama vile U.T.I
(Urinary Tract Infections), na pia huweza kusababisha magonjwa ya figo na
mchafuko wa damu, (bacteremia).
Kuna hali huwa inajitokeza kwa baadhi ya watu, yawezekana
alikuwa kabanwa na mkojo au alikuwa hajahisi kwenda kukojoa, ila akinywa maji
au akisikia sauti ya maji yanachuluzika mfano maji yakitoka bombani, basi
atahisi kwenda kukojoa.
Mpenzi msomaji, ni vyema tukawa wasikivu pale mtu unapobanwa na haja (mkojo), hii ni kwa ajili ya afya ya kibofu chako cha mkojo lakini pia ni kwa
ajili ya afya yako kwa ujumla. Kama unalo tatizo, usisite kuonana na wataalamu
wa afya..
Monday, 17 August 2026
ELEWA CHANZO CHA FIGO KUSHINDWA KUFANYA KAZI (KIDNEY FAILURE)
![]() |
| Picha na: Ahli Hospital |
FIGO ni miongoni mwa viungo muhimu sana katika mfumo wa utendaji
kazi wa mwili wa binadamu. Wiki iliyopita nilieleza jinsi kiungo hiki
kinavyopata mawe na jinsi ya kujikinga na tatizo hili.
Chanzo: Global
Nashukuru wengi wamepiga siku kushukuru kwa elimu ile. Kwa
kawaida, mwili wa binadamu una figo mbili zenye maumbo yanayofanana kama yale
ya maharage, yakiwa yamejificha nje ya utando unaozunguka tumbo, chini kidogo
ya mbavu za chini.
Kazi kuu za figo ni kuchuja vitu mbalimbali pamoja na sumu
katika damu na hivyo kusaidia katika kuhifadhi na kuthibiti kiwango cha maji na
madini (electrolytes) mwilini.
Katika kutekeleza hayo, figo huchuja vitu hivyo pamoja na maji
yaliyo mwilini na kutengeneza mkojo, huchuja pia maji yasiyohitajika mwilini
huku yakinyonya madini na kemikali muhimu kuzirudisha katika mzunguko wa damu
na kutoa nje uchafu usiohitajika.
Kazi nyingine za figo ni kurekebisha na kuthibiti kiasi cha vitu
mbalimbali katika damu pamoja na kiasi cha maji katika mwili, husaidia
kutengeneza kiasili cha erythropoietin ambacho ni muhimu sana katika
utengenezaji wa chembe nyekundu za damu, husaidia uzalishaji wa vitamini D na
husaidia pia katika kuthibiti na kurekebisha shinikizo la damu mwilini (blood pressure).
Kwa kawaida damu inayozunguka mwilini hatimaye huingia kwenye
figo kwa ajili ya kuchujwa, kutoa uchafu pamoja na sumu nyingine zisizohitajika
mwilini.
Kitendo hiki cha utengenezaji mkojo hufanyika katika hatua kuu
zifuatazo;
Hatua ya kwanza ni UCHUJAJI.
Damu kutoka nje huingia ndani ya mafigo na kupita kwenye
glomeruli, lenye umbo kama chekeche/chujio ambalo limeundwa na mishipa mingi
midogo ya damu iliyojizungusha pamoja.
Vitu mbali mbali, maji pamoja na sumu zilizo katika damu
inayopita kwenye vimishipa hivi na kisha kuingia katika mirija mingine mikubwa
kwa ajili ya uchujaji zaidi.
Mirija inayofuata huendelea kuchuja damu na kunyonya baadhi ya
vitu vilivyo chujwa kimakosa kuvirudisha mwilini, mpaka kiasi sahihi cha uchafu
kinachotakiwa kuchujwa kinapokuwa kimefikiwa.
Mara baada ya mkojo kutengenezwa na kutolewa kwenye figo,
husafiri kuingia kwenye kibofu cha mkojo kwa kupita kwenye mirija ijulikanayo
kama ureta.
Kutoka kwenye kibofu, mkojo hutolewa nje ya mwili kupitia kwenye
mrija wa urethra.
Kushindwa kufanya kazi kwa figo hutokea iwapo sehemu ya figo au
figo lote litapoteza uwezo wake wa kuchuja maji na uchafu kutoka katika damu na
kutengeneza mkojo.
Kitendo hiki husababisha kusanyiko la uchafu pamoja na sumu
kadhaa katika damu ambazo ni hatari kwa afya ya mhusika.
Figo kushindwa kufanya kazi kumeganyika katika makundi
yafuatayo, Figo kushindwa kufanya kazi kwa ghafla (Acute Renal Failure (ARF),
Figo kushindwa kufanya kazi kwa kiasi (Mild renal/kidney insufficiency) na
tatizo sugu la figo kushindwa kufanya kazi (Chronic renal failure).
Figo kushindwa kufanya kazi kwa ghafla (Acute Renal Failure
(ARF) Hii ni hali inayotokea kwa ghafla, na kudumu kwa saa chache mpaka siku
chini ya 14, na kusababisha ongezeko la kiwango cha creatinine na urea katika
damu.
Hali hii huwapata karibu asilimia 5 ya wagonjwa waliolazwa
hospitali kwa sababu ya matatizo mbalimbali. Aidha hali hii hutokea zaidi kwa
wagonjwa mahututi na wale wanaohitaji uangalizi wa kipekee, yaani waliolazwa
ICU.
SABABU ZAKE
Visababishi (au aina) vya ARF vinaweza kugawanywa katika makundi
makuu matatu: Matatizo yanayoathiri mtiririko wa damu kabla ya kuingia katika
figo (Prerenal causes/failure), matatizo ndani ya figo lenyewe yanayozuia na
kuathiri uchujaji wa damu au uzalishaji wa mkojo (Renal causes/failure),
matatizo yanayoathiri mtiririko wa mkojo nje ya figo (Postrenal causes/
failure)
Matatizo yanayoathiri mtiririko wa damu kabla ya kuingia katika
figo (Prerenal causes/failure) Aina hii hutokea kwa takribani asilimia 60 mpaka
70 ya ARF zote. Katika kundi hili, figo hukosa damu ya kutosha kwa ajili ya
kuchuja na hatimaye hushindwa kufanya kazi yake ipasavyo. Mambo
yanayoweza kusababisha pre-renal failure ni pamoja na:
Upungufu wa maji mwili unaosababishwa na kutapika kupita kiasi,
kuharisha, au kupoteza damu kupita kiasi (kwa sababu ya ajali au kuumia),
kuvurugika kwa mtiririko wa damu inayoingia kwenye figo kwa sababu ya: Kushuka
kwa ghafla kwa shinikizo la damu kwa sababu ya kupoteza damu nyingi wakati wa
upasuaji mkubwa, kuumia au kuungua sehemu kubwa ya mwili, au maambukizi katika
mfumo wa damu (sepsis) yanayoweza kufanya mishipa ya damu kutanuka na kushusha
shinikizo la damu, kuziba au kusinyaa kwa mishipa inayopeleka damu kwenye figo.
Figo inaweza kufeli pia kutokana na moyo kushindwa kufanya kazi
(heart failure) au shambulio la moyo (heart attack) linalosababisha kushuka kwa
shinikizo la damu na ini kushindwa kufanya kazi (liver failure) kunakoweza
kusababisha mabadiliko katika mfumo wa homoni zinazoathiri shinikizo la damu
pamoja na mtiririko wa damu kwenda kwenye figo.
Mwanzoni kabisa mwa pre-renal failure huwa hakuna athari yoyote
inayotokea kwenye figo, na mara nyingi, figo laweza kurudi katika hali yake ya
kawaida iwapo chanzo cha tatizo kitagunduliwa na kushughulikiwa ipasavyo.
Mambo yanayosababisha madhara katika figo husababaisha karibu
asilimia 25 mpaka 40 ya vyanzo vyote vya ARF. Visababishi vilivyo katika kundi
hili hujumuisha vile vinavyoathiri uchujaji, mtiririko wa damu ndani ya figo na
seli za figo zinazoshughulika na uchujaji na ufyonzaji wa chumvi na maji.
Visababishi hivyo ni pamoja na: Magonjwa katika mishipa ya damu,
kuwepo kwa damu iliyoganda ndani ya mishipa ya damu inayopita katika figo,
ajali/ Kuharibika kwa tishu na seli za figo, magonjwa ya mzio katika glomeruli
na figo kwa ujumla (glomerulonephritis).
Magonjwa yanayoweza kusababisha hali hii ni pamoja na maambukizi
(infection) ya bakteria jamii ya streptococci.
(More: Here Endelea kusoma hapa)
Wednesday, 15 February 2023
BAADHI TABIA HATARISHI ZINAZOFANYA MTU KUTOKUELEWEKA KATIKA UHUSIANO.

Image copyright: fakazanews
Na. Stewart Meena
Mahusiano siku
hizi za karibuni yamekuwa na chagamoto nyingi sana kiasi kwamba Watu
wanapoingia katika mahusiano (Uchumba) inakuwa kama kila mmoja ana mashaka na
mwenzi wake kuwa je ana malengo ya kufanya maisha pamoja ama yuko kwa sababu ya
jambo Fulani na anapita tu baada ya muda hudai kuachana.
Kisaikolojia:
Mwanamke hupenda kwanza kasha mengine hufuatia baadae, tofauti na Wanaume wao
hutamani kwanza kasha kupenda huja baadae “Yaani kupenda kwao hutokea ndani ya
huo uhusiano, alikotamani kwanza” na hapa ndipo bahati mbaya kwa Wanawake
huwaona Wanaume zao kama hawaeleweki, lakini pengine Wanawake hawa wameshindwa
kuchunguza mambo ambayo Mwanaumeze wake hupende, kasha aishi humo na baadae
kueleweka na kupenda kwa Mwanaumehuja tu moja kwa moja (Automatic)
Tabia za mwanaume
zinazochagizwa na kuwa na mwanamke kwa kumtamani kwanza ndio hupelekea mwanamke
husika amuone mwanaumw wake ‘Haeleweki’ kasha hujikuta amefanya maamuzi ya
kumuacha Mwanaume wake, na kwenda sehemu nyingine, mpaka pale atakapopata huyo
anayedhani kwake anaeleweka".
Bahati mbaya ni
kuwa kwa kutokufahamu kwake, tatizo halipo hapo kwa (Mwanaume wake haeleweki)
ila lipo hapa kwenye kufahamu Mwanaume wake nini anapenda kutoka kwake kwenye
hayo mahusiano, na ni vipi mwanamke huyo ajiweke vile ambavyo mwanaume wake
anavyopenda ili kutengeneza Uhusiano imara na wenye kuzaa matunda ya ndoa na
Familia.
Kimsingi: Ulishawahi
kusikia Kauli Kama hizi Kwa wanawake, wakisema mwanaume Yule haeleweki, Mpenzi
wake haeleweki, au hata wale walio kwenye ndoa utasikia pia wanasema Mume wake
haeleweki, mchumba wake haeleweki nk.
Nachotaka
kuwakumbusha Wanawake na Wanaume ni kuwa: Mwanaume hutamani kwanza kasha kupenda
huja baadae; na Mwanamke hupenda kwanza kasha kutamani kuwa na huyo mwanaume
huja baadae, ‘Ndio maana wahanga wakubwa wa hii KUTOKUELEWEKA’ ni wanawake
zaidi ya wanaume sababu tayari wameingia sehemu kwa kupenda kwanza, na walicho
kitegemea ni tofauti sana na wanaume zao walichokiwaza.
WANAWAKE WASEMAPO
‘Mwanaume haeleweki’ HUMAANISHA HAYA
YAFUATAYO:
- Mwanaume ameshindwa kumfanya ajione yupo pekeake moyoni mwake, na pia hana uhakika yeye ndio utaolewa.
- Mwanaume kutoa mara kwa mara zisizotimilizika, Wanawake hupenda kuwajaribu wanaume zao kwenye ahadi wawapazo.
- Mwanaume kuficha chanzo cha kipato chake kwa Mwanamke wake, na hivyo kumfanya Mwanamke wake kushindwa kujua siku Mwanaume wake akiwa na pesa ama asipokuwa na pesa, hivyo anakuwa hana uhakika na huduma atakazozipata pindi atakapoolewa.
- Mwanaume kuficha shughuli azifanyazo, kuficha ndugu zake, marafiki zake kwa Mwanamke husika kwa kutokutaka mwanamke huyo atambulike kwao,na kumwambia sio wakati sahihi kutambulishwa, kwa kuwa bado ana hofu ya kutambulisha kasha baadae kuachwa solemba hivyo ni kama na yeye anatega-tega hivi.
- Mwanaume anayepoteza kumbukumbu za matukio muhimu kwa mwanamke wake, hupelekea kutoeleweka na mwanamke husika hushindwa kuelewa wanathaminiwa na kupendwa ama laah. “Wanaume wanaopoteza kumbukumbu hasa zile za muhimu kama birthday zao, Ahadi wazitoazo nk, Mwanamke hufikiri Mwanaume wake hamjali.
![]() |
| Image: ThePrint |
HIVYO: Katika mahusiano (Uhusiano) Mwanamke anahitaji kwanza ‘Life Security’ kama ‘Kuthaminiwa, Kupendwa yeye pekeake, kuhudumiwa mahitaji yake mbalimbali, Kutunzwa au kupewa kipaumbele kwanza na (Kudekezwa – Hii ipo kwa wote wawili).
WANAUME:
Kadhalika, hupendelea kufanyiwa yale wawafanyiao wenza wao, na wasipofanyiwa
huanza kuwa na mashaka na sehemu waliyoko na kukaa nusunusu (Kwa mashaka) na
kuwaza kuachana muda mwingi sababu tunaishi kwenye Dunia ambayo kuachana
imekuwa ‘Faheni’
WANAUME WASEMAPO ‘Mwanamke haeleweki’ HUMAANISHA HAYA
YAFUATAYO:
- Mwanamke kushindwa kumfanya mwanume ajione yupo pekeake kwako, na hata iweje huwezi kumsaliti kwa wengine sababu unafaa kuaminiwa na ni mwanamke unayejiweka mbali na mambo ya anasa kama Pombe, Starehe, kwenda club nk. Lazima Mwanaume wako asikuelewe sababu mazingira kama hayo kumsaliti ki tendo la dakika1 tu.
- Mwanamke, kutamani kila jambo zuri ufanyiwe wewe tu, na wewe huna hata siku moja unayotamani kumfanyia mwanaume wako mambo hayo mazuri wewe unayotaka ufanyiwe. Mfano: Kutafutwa kwa simu, wewe ndio utafutwe tu, vijizawadi wewe ndio upewe tu, kusifia wewe ndio usifiwe tu, birthday wewe ndio ikumbukwe tu na ufanyiwe, khaa! Kwani yeye sio mja (Binadamu!?) Lazima mwanaume wako ahisi hufurahii yale ambayo anakufanyia.
- Mwanamke kufuja fedha, yaani wewe hujui kama kuna kupunguza matumizi yasio ya lazima sana, hujui ‘kuSave’ kwa ajili ya kesho au maisha yenu ya siku zijazo, wewe kila siku ni kuitisha vitu tu vya gharama, badala ya kupika mle nyumbanikila siku unataka mitoko ya hoteli kubwakubwa-, sawa utapewa yote hayo lakini mwisho wa siku mwanaume huyo utamuona haeleweki kwako, punde akishakutumia. ‘Wanaume hupenda na hutulia kwa Wanawake wanaoifikiria kesho yao’
- Kama ilivyo kwa Wanaume, Mwanamke kuficha kipato chake, kushindwa kumsaidia mwanaume wake hata kwa mambo madogo-madogo, lazima taa nyekundu iwake kichwani kwa Mwanaume husika “Yaani Mwanaume anaweza kukwambia hata kwa kukutega-naumwa, sina hata pesa ya kwenda kupima, na wewe kwa kujitutumua unamwambia ‘Pole utapata, badala ya kumwambia ngoja tufanye maarifa, au nna elfu5 hapa tafuta ya kuongezea, au ngoja nikuletee paracetamol utilize maumivu nk. Mwanaume lazima akuone hueleweki na mwishowe hutafuta huyo atakayeeleweka.
HIVYO: Katika
mahusiano (Uhusiano) Mwanaume kamailivyo kwa Mwanamke, naye anahitaji kwanza ‘Love
Security’ tofauti na Mwanamke anahitaji kwanza (Life Security), kama
‘Kuthaminiwa, Kuonyeshwa anapendwa pia, kutekelezewa huduma na mahitaji yake
mbalimbali ya msingi, Kupewa kipaumbele kwanza kabla ya ndugu zako na marafiki
zako, na zaidi kumsikiliza kwa yale anayotaka ufanye na yale asiyoyataka
usifanye. (Wanaume hupenda sana kusikilizwa na kupewa nafasi ya kuwa kiongozi
wa uhusiano wenu, na sio kupandwa kichwani n.k).
WANAWAKE: Huwaelewa
wanaume wanaotimiza ahadi hasahasa ahadi ndogondogo kwani kupitia kutimiza
ahadi kunamfanya akuamini na azidi kukupenda, yaani ni Bora usimuahidi jambo
lolote kuliko utoe ahadi ambazo utashindwa kuzitimiza, jambo ambalo yeye analichukulia
Kama Deni.
Fikiria: Unapenda mwenza wako akufanyie nini,
hivyo upendavyo vivyo hivyo Mwanza wako naye hutamani wewe umfanyie hay ohayo “Na
ukimfanyia atafurahia vile ambavyo wewe ufurahiavyo”
MWISHO: Wanaume wenye kufikiria kutumia
mabavu, Maneno machafu, makali au Kauli za vitisho na Kuhisi mabaya kwa
mwanamke wake, “Mfano, kumwambia – Unachepuka eeh, ondoka kwenu, nitakupa talaka,
nitaongeza mke mwingine n.k” huwanyong’onyeza wanawake husika na kujiona hawako
sehemu sahihi, sababu Wanaume wanachopaswa kufahamu ni kuwa “Wanawake huamini maneno
zaidi kuliko hata matendo” yaani Kadiri unavyomtisha mwanamke wako unamtengezea
mazingira ya kujihami na kujiandaa Kwa lolote ‘Kuachana, Kuchepuka nk’.
Kama ilivyo kwa Wanawake, Wanaume pia hawapendi kuishi na mtu wasiyemuelewa, kwani kila mmoja hufikiria usalama wake kwenye huo Uhusiano, hufikiria kumpata mtu sahihi wakufanya naye maisha na atakaye mthamini katika wakati wa shida na raha hadi umauti umfike mmojawapo.
Tafadhali, uchukuapo na kunakili makala tambulisha na blog hii: Saysteefeatures.blogspot.com" asante; Share Makala haya na Wengine wapate kuelimika zaidi kuboresha mahusiano yao.
Source: (Msaada wa Mitandao Washirika)
Tufuatilie Mitandao ya Kijamii:
Facebook: www.facebook.com/stewart.meena
Instagram: @ Master The Last
Saturday, 29 January 2022
ZITAMBUE SIKU MAALUMU KUPATA UJAUZITO NA SALAMA ZISIZOTUNGA MIMBA
Friday, 2 July 2021
FAHAMU: FAIDA LUKUKI KIAFYA KUWEKA KITUNGUU MAJI KWENYE UNYAYO WA MIGUU
Monday, 24 August 2020
JE! WAIFAHAMU AFYA YAKO KUPITIA RANGI YA MKOJO (Urine Colour)?
![]() |
| Picha kwa hisani ya mtandao (Google search) |
Na Stewart Meena
Je unafahamu ya
kwamba rangi ya Mkojo wako (Ashakhum sio matusi nitatumia jina lake halisi
badala ya kupunguza ukali wa maneno kusema "haja ndogo" ili tuelewane) inakupa
matokeo sahihi kuhusu hali ya afya yako?
Lakini pia wajua maji
ndio afya yako! Kwa sababu asilimia kubwa ya ufanyizo wa mwili wako ni maji
(Yaani damu+maji) na asilimia 25% ni mjumuisho mwingine kwenye mwili wako, mfn.
Nyama za ndani na nje nk.
Kama jibu ni hapana basi
"MAKALA HII" inakusu wewe moja kwa moja; Kwani rangi ya mkojo kwa
mujibu wa watalamu wa afya kupitia mahojiano mbalimbali niliyoyafanya na madaktari
na wataalamu wa tiba za asili, pamoja na tafiti zangu zingine nlizozifanya kwa
kuandika, au kusoma vitabu na majarida mbalimbali yahusuyo Afya:
(Nikiwa
Fani yangu ni Mwandishi wa Habari)
Nimekuja na majibu
kuwa kupitia Rangi ya mkojo wako unauwezekano mkubwa na ndio kipimo sahihi
kinachoweza kukupa ukweli wewe juu ya afya yako, kuweza kujua dalili za awali
kabla hata ya kwenda kupima maabara au kufanyiwa uchunguzi wa vipimo na
daktari.
Ndio ili daktari ajue
wewe unaumwa nini, au niugonjwa gani unakusumbua kwa wakati huo "ukiacha scanning na kupigwa picha ya
X-rays" Daktari huitaji kupima damu yako kwa matatizo ya nje ya mfumo wa
tumbo lako au kupima haja ndogo (mkojo) na (haja kubwa) ili kujua matatizo ya
ndani ya mfumo ulioko tumboni mwako.
Asilimia takribani
75% kwa 25% ya mwili wako ni maji, damu na nyenzo mwili nyingine, na vyote hivi
hufanya kazi kwa pamoja katika kuendesha maisha ya muhusika na ikiwemo mwili
kujitengenezea kinga yake ya kutosha na muhusika kuishi kwa afya bora.
Naposema matatizo ya
ndani ya mfumo uliopo tumboni (namaanisha magonjwa ambayo tunayahisi kupitia
eneo la tumbo letu) Kama vile, maumivu ya tumbo na yanayoweza kuambatana na vichomi
vya mara kwa mara, ambayo haya huweza kusababishwa na maradhi-mwili kadhaa ya mfumo
huo kama vile typhoid, amoeba,
Vidonda vya tumbo, matatizo ya figo na ini, Safura, kansa ya utumbo, Chango na
ngiri nk.
HEBU NA TUJADILI SASA
UTAMBUZI WA AFYA YAKO KUPITIA RANGI YA MKOJO.
Maelezo Mengine Kwa
kina:
![]() |
| Picha kwa hisani ya mtandao (Google search) |
Kwa kawaida mkojo
tuutowao una rangi mbalimbali (pichani) zenye majina yake kufuatana na rangi au
muonekanao wake, Na hiyo huchagizwa na mazoea ya mtu kuijali afya yake au
kuipuuza afya yake kwa kujua au kutokujua.
(Ndio mbona uvutaji
wa tumbaku au sigara na unywaji wa pombe kupita kiasi ni hatari kwa afya yako,
na imeandikwa hivyo lakini bado watu wanakunywa pombe kupitiliza na kuvuta
tumbaku!?).
Sawa, sasa na hebu
tuanze kuzichambua rangi hizo (Pichani) na
ZINAVYOASHIRIA KWENYE AFYA YA MWILI WAKO.
No1. (Transparent)
Mweupe kabisa au
Mkojo usio na Rangi ya mkojo (Light yellow): Inaashiria Unakunywa maji mengi
sana, na sumu iliyoko katika mwili wako inasafishika vyema, Kwani figo yako kwa
msaada wa maji mengi mwilini huchuja sumu na taka mwili vyema kwa kutenga virutubisho
mwili na taka-mwili.
Kiafya, mkojo wa rangi hiyo (Nyeupe kama maji) sio
mzuri sana na huweza kuwa kwenye mwili wako kuna kasoro fulani au mmeng’enyo na
huenda uchakataji wa virutubisho na kuondoa sumu mwili haiko sawia kwako (balanced)
KIAFYA: Binadamu
anapaswa kunywa walau glasi 8 za maji kwa siku hadi lita mbili, na sio pungufu
kwa faida za kiafya, hivyo kunywa maji pia kupitiliza huleta matokeo mengine
tofauti kiafya.
Hivyo unashauriwa, utakapoona mkojo wako hauna rangi ya mkojo yani unatoka mweupe kama rangi ya maji hapo Kiafya kuna jambo haliko sawa (balanced) kwa hivyo unatakiwa aidha kupunguza kidogo unywaji mwingi wa maji au kuzingatia ulaji sahihi vya virutubisho mwili (balance-diet)
No2. (Lemonade) Hiyo
ni Excellent / great / better / Very good
Manjano isiyokoza
(Light yellow) inaashiria unakunywa maji
ya kutosha, afya yako iko vizuri na imara, hauna matatizo yoyote hivyo endelea
kufanya unacho kifanya kwa kula vyakula "balanced-diet", kula matunda
na kunywa maji mara kwa mara.
KIAFYA: Wewe unashauriwa
ushikilie hapo hapo katika utaratibu wako wa maisha ya kila siku "life
style" kwani mwili wako unajiendesha vyema.
Ili Kupata matokeo
haya: Unapaswa kula vyema vyakula vyenye virutubisho mwili vyote
(Wanga+Protini+Vitamini) ikiwemo na matunda kwa kuzingatia ulaji sahihi
(Balance diet) pamoja na unywaji wa maji mara kwa mara hata pasipo kuhisi kiu
(isipungue glasi 6-10 kwa siku)
No3. (Light like a
beer)
Majano isiyokoza
(yellow) yaani rangi halisi ya mkojo, inayokaribia kufanania na rangi ya asali
na isiyotoa harufu kali, inaashiria afya yako kwa wakati huo haina matatizo yoyote
na unazingatia ulaji mzuri wa vyakula na unaupenda mwili wako, #Isipokuwa
tatizo lako ni kuwa sio mnywaji mzuri wa maji ya kutosha vyema hivyo mwili wako
hauna maji ya kutosha.
KIAFYA:
Ukiona hivyo hupaswi
kuwa na wasiwasi, kwani kwa unywaji wako mdogo wa maji bado mwili wako
unajitengenezea maji ya kutosha pengine kutokana na aina ya vyakula uvilavyo
pia.
Isipokuwa unashauriwa tu kuongeza unywaji wa maji zaidi kwa siku kabla ya kula na baada ya kula unatakiwa usubiri angalau dakika20-30 hata kama hauna kiu ili kurahisishia figo yako ufanisi wake zaidi.
No4 (Amber) that is
Bad/Warning
Manjano
iliyochanganyika na uKijani kwambaali (Amber) Inaonyesha mwili wako upo upo
"kawaida" na una afya ingawa si mnywaji wa maji mengi na unasubiri hadi
uhisi kiu ndio unywe tena kidogo ndio maana unapokojoa mkojo hutoka na harufu
kali, hauzingatii ulaji wa virutubisho-mwili sahihi (yani wewe hauli
balance-diet kwa kuegemea aina ya vyakula fulani pekee na mara kwa mara, haswa
vile venye rangi ya uKijani kama mbogamboga na matunda" (mwili
unatengeneza vitamini na wanga pekee), ila kwa uchache unywao Mwili wako una
maji ya kutosha.
KIAFYA: Ukiona hivyo
ni ishara ya tahadhari au onyo mwili wako unakupatia ujumbe kuwa kuna kitu au
jambo haliko sawa mwilini mwako hivyo yakupasa ubadili mfumo wako wa maisha
mara moja; pia unatakiwa uzingatie unywaji wa maji hata pasipo kuhisi kiu,
pamoja na kula kwa kuchanganya vyakula vyenye kuupatia mwili wako madini ya
protini kwa wingi na Vitamini-C.
Protini inapatikanaje!?
Hii hupatikana kwa kula vyakula kama Nyama nyekundu (Ng'ombe, mbuzi nk) pamoja na vitu kama Maharagwe, samaki, maziwa nk.
No5 (Very bad /
Worse)
Manjano iliyochanganyika
na nyekundu au rangi ya udongo (Brown) isiyo na harufu kali ya mkojo na yenye
harufu kali au ya wastani, Inaashiria Upo kawaida tu ila mashakani, sababu wewe
kwanza si mywaji wa maji, pili hauzingatii ulaji sahihi wa chakula na pengine
hauli kwa muda sahihi pia na upo hatarini kupatwa na Vidonda vya tumbo (ulcers) Tatu,
kuna aina ya kemikali unazokula au kunywa na kusababisha mwili kukaushwa maji
yake kwa wingi zaidi.
KIAFYA:
Kunywa maji ya
kutosha kwa siku mbili au tatu, na kama hali ikiendelea hivyo yakupasa umwone daktari
upesi kwa vipimo vya mkojo wako kujua kama una UTI, baikteria mwilini waletwao
na unywaji wa maji machafu "typhoid" nk.
LABDA NIELEZEE HAPA
KIDOGO:
Kuna aina ya vinywaji
na vyakula tunavyokula ambavyo huweza kufyonza maji-mwili kwa wingi zaidi au
hata kazit unazozifanya kwa kupata mkate wetu wa kila siku.
Mfano kazi za kutumia
nguvu sana, kukaa karibu na moto kwa muda mrefu zaidi, kufanya kazi viwandani
haswa vile vyenye kutumia nishati ya umeme au moto na makaa ya mawe nk.
Kutembea kila siku
umbali mrefu tena juani kwenda na kurudi; kubeba mizigo mizito nk inafyonza
sana maji mengi mwilini.
Ukiwa mpasuaji mbao
kunywa maji yakutosha, ukiwa unafanya kazi ya upishi hakikisha unakunywa maji
ya kutosha tena mara kwa mara, ukiwa fundi ujenzi, makenika, injinia, dereva,
mbeba mizigo mizito, mfanyaji mazoezi mara kwa mara, mwana michezo, mchumia
juani nk. Hakikisha chupa ya maji haibanduki pembeni yako na unakunywa maji
mengi mara kwa mara.
Ndio maana wataalamu
wanasema na kushauri: Ikiwa unaishi kwenye ukanda na mikoa yenye joto kali (Dar
es Salaam, Tanga, Pwani, Morogoro,
Dodoma, Mara, Mwanza, Singida, Mtwara, Kilimanjaro "sehemu baadhi"
nk) yakupasa unywe maji mengi kwa siku kwa sababu maeneo hayo humfanya muhusika
kutokwa na jasho jingi kupita kiasi hata bila kufanya kazi nzito au kufanya
mazoezi.
Kutokunywa maji hayo
hupelekea mwili kudhoofu, kuharibu mfumo mzuri wa uchujaji wa sumu mwili,
chakula kutokusagika na kuchaguliwa vizuri nk. Na ikidumu hivyo kwa muda mrefu
ndipo mtu unaweza kupatwa na #magonjwa hatari zaidi kama vile figo kufeli,
kupata vidonda vya tumbo, ini kuungua, Kinga za mwili kushambuliwa na magonjwa
mengi zaidi na kwa mjumuisho wa hayo yote na pasipo kupata suluhisho la
kitabibu kama kumuona Daktari kinachofuatia ni kifo tu
hakuna cha ziada.
Muhimu kutambua ni
kuwa: Mwili wa Binadamu hutegemea kupata maji yake kupitia pia aina ya vyakula
unavyokula kila siku, matunda, vinywaji, maji yenyewe na virutubisho-dawa,
ambapo kwa mjumuisho wavyo mtu huweza kuwa na maji ya kutosha mwilini, kuwa na
afya njema, kinga za mwili kufanya kazi sawia, na Kupambana na maradhi
nyemelezi, mwisho maradhi shambulizi yatakupitia pembeni (utayasikia kwa jirani
tu)
Mwili unafanyizwa na
seli mbili za damu (nyeupe na nyekundu) ambazo hizi ndio ngao zetu, kinga na
ndio huyafanya maisha yetu yasonge.
Ndio maana
ukipungukiwa na damu wewe ni wa ICU, ukipungukiwa na maji wewe ni wa ICU pia na
uzembeaji kidogo, malaika mtoa roho utamuona akipita pembeni yako mara kwa mara.
(NDUGU ZANGU AFYA NI
MALI NA NI UHAI WAKO USIUCHEZEE
Swali la kujiuliza
kabla ya kuhitimisha ni kuwa: Je! Unawezaje kuchezea uhai wako na afya yako!?
Binadamu huchezea
afya yake na kuhatarisha uhai wake kwa kufanya mambo mbalimbali (mengi
unayafahamu) na ndio maana unaweza kumsikia mtu akisema maisha yenyewe mafupi
haya!?
Sababu anafanya jambo
ingawa anatambua madhara yake, na hii ni kweli kabisa watu wengi walioelimika Wasomi
ndio haswa huongoza hapa: ni walevi wa pombe kali, watumiaji wa madawa ta
kulevya, hawazingatii ulaji sahihi na kwa wakati hupuuzia taarifa kama hizi
(uisomayo) na mwisho wa siku pyuuuuuuu!
They disappear forever!
Sio ajabu kizazi
chetu cha leo (karne ya 21) kumuona kijana umri mdogo kabisa lakini Kimuonekano
kashaZeeka kabisa, ndio si tunawaona mtaani huko!?
Wazee wetu (miaka ya
60, 50, 40, kurudi nyuma) ukiwaona leo hii bado ni imara licha ya changamoto ya
maisha na umaskini na huwezi kuwasikia wakiwa na matatizo kwa wingi kama
tuliyonayo vijana wa miaka hii (80, 90, 2000 kuja mbele) ambapo magonjwa kama
presha, kizukari, miguu kuvimba, utasa, kupoteza nguvu za kiume, yote haya anayo
mtu mmoja..
HIYO NDIO KUCHEZA NA
AFYA NA UHAI WAKO PIA.
Ndio! Ukipatwa na
hayo yote mwisho wa siku unafikiri nini kinafuatia!? Saa nyingine hebu tuache
kumbebesha MUNGU lawama na mizigo asiyostahili, amekupa maarifa ya kutambua
mema na mabaya yatumie!?
Acha kuwa kichwa_maji
(ashakhum sio matusi) Huwezi ukaambiwa unywaji wa pombe kupitiliza ni hatari
kwa afya yako bado unakunywa! Tumbaku, bangi, cocaine ni hatari kwa afya yako
bado unavuta!?
Kunywa maji mengi
bado hunywi!, kula mlo kamili (balance diet) bado huli wakati afrika
tumejaaliwa vitu vyote hivyo, ungekuwa unaishi jangwani (deserts) ungesemaje!?
Wewe si mnywaji wa
maji, hivyo Endelea kunywa maji ya kutosha walau glasi 4-8 au zaidi kwa siku,
ukipata #Stakafeli kula, juisi ya Miwa, ndizi, nanasi, chungwa, limao,
tangawizi, karafuu, nazi, mihogo, #maharagwe, viazi "sio vya kukaanga na
mafuta" kula.
Embe, limao, nyama,
bamia, mboga za majani kulaaa-uwiiiiii!
Hahaha! Vingine unavijua! (Muhimu hakikisha mlo wako unajumuisha virutubisho na
madini ya - Vitamini, wanga na protini)
Makala zinazofuata,
ntajaribu kukuorodheshea baadhi ya vyakula na matunda ambavyo huweza kuupatia
mwili vitamini, wanga na protini.
KUMBUKA: Rangi ya mkojo inayotoka na “Uwekundu (mfano wa damu) na mkojo unaotoa harufu (Red urine colour) Ndugu yangu hapo kimbilia kituo cha Afya kilichopo karibu na wewe, na sio kuendelea kukaa nyumbani na kutumia muzugwa, dawa za miti shamba (hapo punde tunaweza kukuimbia ule wimbo wa parapanda)
RANGI HIYO KIAFYA: Mwili
Upo kawaida (sababu bado unaweza kujihisi una nguvu kiafya) ingawa sumu mwili
iliyopo katika damu haichujwi vyema na kusafishika na figo
zako, yaani Ini
limekataa kufanya kazi yake, hivyo madhara ya hivi muda mrefu huweza kuzalisha
matatizo katika figo zako kufa kabisa, kupata vichomi vya mara kwa mara, tumbo
kuuma, mwili kuishiwa nguvu nk.
HEBU SOMA HAPA KUHUSU
KUJUA KAMA FIGO ZAKO ZINA HITILAFU:
MKOJO wenye Rangi ya
Pinki, damu ya mzee na inayokaribia kuwa kama Nyekundu
(Blood colour). Kama
hujala matunda yoyote, chakula, au kinywaji chenye asili ya uwekundu kwa
wingi" (juisi ya rangi, ubuyu wa rangi nk)
Au Mwanamke haupo kwenye
siku zako za hedhi (ashakhum sio matusi)" basi huwenda una matatizo makubwa
kwenye mwili wako, ambapo damu hulazimika kuchanganyika na njia ya mkojo
"kwenye kibofu chako cha mkojo".
Ukiona dalili hiyo
tambua kuwa Inaweza ikawa sio ishara mbaya kwa mara moja ila ikijirudia kwa
muda wa siku zaidi ya 2 au 3 ni tatizo hilo, tena lenye kuhitaji vipimo na
matibabu ya kidaktari upesi zaidi.
Muone daktari haraka
sana Ufanyiwe Vipimo kujua kama, unakabiliwa na magonjwa yepi.
LABDA NIELEZEE KIDOGO
HAPA:
Mara nyingi (sio
zote) mkojo kutoka na rangi ya kama damu huwa inachagizwa na kuchanganyika na
damu, na hadi ikitokea hivyo zaidi ya mara2 au siku2, (Isipokuwa wanawake
wakati wa hedhi) basi kuna jambo ambalo halipo sawa mwilini. "Mwili una
dosari fulani)
Na huwenda muhusika anakabiliwa
na magonjwa kama vile ya zinaa (mf.Kaswende, pangusa nk); au kinaMama kuwa na
tatizo kwenye mlango wa kizazi "mwanamke", kuathirika kwa ini, tatizo
katika kibofu chako cha kuhifadhia mkojo, njia ya kupitishia mkojo, au pengine
inaweza ikawa ishara ya ugojwa wa Figo, Ini au uvimbe kwenye njia hiyo ya mkojo
nk.
PATA USHAURI WA
KIDAKTARI NA PIMA AFYA YAKO MAABARA AU KITUO CHA AFYA AU KWA KUJICHUNGUZA
MABADILIKO YAKO MARA KWA MARA MWENYEWE HUKU UKIJIPENDA NA KUILINDA AFYA YA
MWILI WAKO PIA.
ENDELEA HAPA ZAIDI (Chanzo kingine):
Tafadhali waweza tufuatilia pia Facebook kwa page yetu ya: (FB-Page)











