Thursday, 10 September 2026

KIVUMBASI: Mmea asilia wa Maajabu katika Tiba

Image right: Earth Living

Mmmea uonao pichani unaitwa Mvumbashi au "Kivumbasi" kiswahili, Kihehe-lwenyi, ormanyunyukwai (kiMasai) Mzumbasha kwa wasambaa na wambugu (Lushoto Tanga), Wengine huyaita: Luvumbampuku, Kivumbani, Mrumbavasi-Upareni, nk. Lakini kwa lugha ya kisayansi (Scientific name) huitwa Tusli 'holy Basil' ukiwa na asili kutoka bara asia nchini India.

Mmea huu uotao kwa mrudikano wa kama kichaka (shrubs) kwa miaka kadhaa imekuwa ikitumika katika tiba asilia, na wengine wakitumia kama kiungo cha chai kwenye unywaji wao wa kila siku, na umetajwa kuleta maajabu makubwa katika kinga na kutibu maradhi mbalimbali katika mwili wa mwanadamu kwenye mazingira yao ya kila siku.

Tuangazie namna unavyotumika katika Tiba asilia:

Hutumika kama kinga ya kufukuza mmbu na nzi katika mazingira yetu na hivyo kutibu Malaria, lakini pia ukinywa juisi yake huelezwa kutibu degedege, ngiri, pia hukata ulevi kwa wanywaji pombe, pia hutibu maumivu makali ya tumbo (Tumbo la kukata/kunyonga) nk.

Kwa degedege la watoto: Unayaweka kwenye maji unayomuogeshea pekee, wengine humnusishia harufu ya majani haya ya Mumbashi:

Mvumbashi huwa na harufu (scent) flani hivi ambapo huponyesha kwa kuivuta tu, ila wengine huichemsha kwenye chai kama kiungo kwa harufu yake nzuri huongeza ladha ya chai.
Lakini pia ukichemsha yenyewe kwa kuchanganya na vifuatavyo hutibu maradhi kama:
 
1)-Kikohozi kwa watoto/mtu mzima.
Chukua majani yake yatwangwe changanya na maji ya vugu vugu kunywa kwa dozi ya 1*2.

2)-Homa ya Malaria
Majani haya yana antipyretic ambayo inaweza kutuliza homa kabisa na kuponesha malaria, Kama ni mpenzi wa chai chukua majani yake yasage kisha changanya na maji ya moto + asali kunywa kama chai.

3)-Kuhara na magonjwa ya tumbo
Majani hayo yana uwezo wa calming mfumo wa utumbo kwa kiwango kikubwa Sana.

4)-Kushusha sukari ya damu
Majani haya yanakinga ya saratani na cholesterol  na kwa watu wenye kisukari hasa wasiotegemea insulin (NID) majani haya yanauwezo mkubwa wa kushusha sukari na kuilinda pancreas inayozalisha insulin kutoharibika.

5)-Kiungulia cha moyo.
Majani ya Scent yamekuwa yakitumika katika kutibu kabisa tatizo la kiungulia, kikohozi, kuhisi mwili vibaya, maumivu ya hedhi, homa, malaria, shida ya kupumua, ukosaji choo, kukosa hamu ya kula, Kichefuchefu na kuboost moyo tiba hii unaweza iyaanda na kuitumia kwa njia ya kunywa kama chai.

6)-Kuongeza maziwa kwa mjamzito.
Chukua majani hayo zaidi ya 20 yatafune na mboga zingine za majani  yatasisimua mfumo wa utokaji wa maziwa kwa kiwango kikubwa

7)-Hufukuza mbali nzi na umbu, hii ni kwa kuyachoma majani yake, ule moshi wake mbu hulewa na kufa.

8)-Hupunguza nicotine inayopatikana kwenye sigara.
Kila baada ya kutumia sigara unachukua matawi kadha unatafuna ili kupunguza kiwango cha nicotine uliyovuta kwenye sigara.
Majani haya yanauwezo wa kupunguza mawazo Yani msongo wa mawazo, mawe kwenye figo.

9)-Hupunguza maumivu ya tumbo.
Majani haya ni zaidi ya vidonge vya aspirin au Panadol kutokana kuwa majani haya hayana side effects maana ni mimea asili.
Pia ni tiba ya kinywa na macho kutokana na kuwa na kiwango kikubwa cha vitamin A.

10)-Tiba ya kuwahi kukojoa na shahawa zisizo na afya ya kuzalisha.

11)-Tiba ya fugus 

Chanzo: 
Dr. William Mtanzania (Usa America) Kwa maoni ya wadau.
TAHADHARI: Matumizi yoyote waone wataalamu wakusaidie, vinginevyo ukiitumia ni kwa hatari yako mwenyewe na sisi hatutahusika kwayo. (It's for your own risk)
🙏 tafadhali like, share pia: comment kama unayafahamu na yanavyotumika ili wengine nao wapate maarifa uliyonayo. (Africa tuna kila kitu basi tu hatujikubali)

Friday, 4 September 2026

POPULAR LAKES IN TANZANIA (BEOND THE MYTH RECORDED AND COUNTING)

Lake Nyasa (Pomonda Rocks)

 Na.

Stewart Meena (writer)

There is article state: Tanzania Said to have fewer lakes "49" in common (Great and small pools lakes-than others East African countries) Ranking 3rd:

Beside Tanzania: The article also exaggerate: Uganda ranking 1st with "69" and Kenya 2nd with "64" Lakes, and small pools lakes.

BUT: What is a real and what is a myth!? (Language used: (Swahili & English)

Remember, Lakes are not like a Rivers, Streams, Glaciers, Marshes or mangroves, and Dams (Which altogether looks alike) "Small pools "mentioned" resembles like a lake" but they are different)

About the article's the numbers in Kenya and Uganda also involves (Small pools, mangroves, Marshes, Dams etc) that why i said "exaggerated number) If you deny it, give us the names, or outline those-that found in your country!

Tanzania Should be Ranking: 1st, Uganda 2nd, and Kenya 3rd, because of the geographical nature of those mention countries, also the total size of those countries' Non deserts zones, &  sources of inland streams that made a lake etc.

In my accounting bellow (Regards Tanzanian mainland) I try to #Mention Lakes, and not including Swamps, Dams or mangroves areas) to establish evidence in that number...

Lets dive In Swahili: Tanzania imefanyizwa na mikoa takribani (26 mainland & 5 in Islands (Zanzibar regions)  na ikiwa imepakana na nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, na Congo DRC, ambazo kwa pamoja zinaunda Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Malawi na Msumbiji upande wa kusini.

Nchi hii ina utajiri wa mbuga za wanyama nyingi zaidi ya 69, ina Mlima mrefu kuliko wote Afrika na wa pili kwa Dunia (Highest standing mountain) KILIMANJARO, na Ecosystem yenye utajiri wa Mito, Maziwa na bahari.

Ni kwa mantiki hiyo basi tunakusogezea baadhi ya Maziwa (Lakes) yanazopatikana katika nchi hii, (Eneo la Tanzania Bara) kama ifuatavyo:

East-africa-map: Peter Hermes Furian

MAZIWA MAKUU (Common Lakes Are): RelatedSource

  1. Ziwa Victoria (likiunganisha mikoa ya Mwanza, Mara na Kagera) huku likichepukia pia katika nchi za Uganda na Kenya. Ni ziwa hili ndio chanzo kikuu cha mto Mara unaokatisha Kenya na Tanzania pamoja na ule mto Nile (River Nile) ambao huu umeambaa-ambaa hadi nchini Misri.
  2. Ziwa Tanganyika (Ziwa lililopo magharibi ya Tanzania na likipitiwa na Bonde la ufa "Great rift valley) na kuunganisha nchi ya Tanzania, Burundi, na Congo DR. Huku ziwa hili inasemekana ni mojawapo ya chanzo cha mto zambezi uliopo nchini Zambia. (Kwa Tanzania likiunganisha zaidi mikoa ya Kigoma, Katavi, Rukwa na Mbeya.) readMore
  3. Ziwa nyasa (Lake Malawi) hili ni ziwa mashuhuri lililopo Kusini mwa Tanzania likiitwa ziwa nyasa upande wa Tanzania na ziwa Malawi upande wa Nchi ya Malawi. Kwa tanzania likiunganisha zaidi mkoa wa Ruvuma na Njombe. Peruzi

 

Lake Kigoma (Kagongo Village  view) By Halidtz

MAZIWA MENGINE NI PAMOJA NA: (eng: Lake = sw: Ziwa) (Geographical Location – HERE)

Lake Natron (Red lake) ziwa lenye magadi, na Maarufu zaidi kwa ndege aina ya flamengo (Kaskazini mwa Tanzania, Mkoani Arusha) HAPA

Lake Natron (Popular for Migrant bird, Flamengo)


Lake chala (Ziwa hili lipo mkoani Kilimanjaro, mpakani kabisa na nchi ya Kenya) Ramani, Mengine hapa ni: Ziwa Kihurio; na Nyumba ya Mungu (God’s house)

Amboseli lake ikiwa Tanzania mpakani na eneo la (Maasai Mara Iliyoko nchini Kenya, mkoa wa bonde la ufa-loitoktok, kajiadoo, kule kunapatikana Hifadhi ya wanyamapori ya Ambussel) hivyo usichanganye na ziwa hili la Tanzania AngaliaHapa

Lake Duluti (Arumeru-arusha)


Ziwa Lutamba; ziwa Maliwe na ziwa Mkoe (Yote yakiwa, Mkoa wa Lindi)

Lake Eyasi (ngorongoro-arusha)

Lake Tenge, (Dar es salaam)

Ziwa Chada; Ziwa Katabe (yote yakiwa Katavi Tanzania)

Lake Kanvi; Kilanga; Tanga; Musimu; Moye; Masimba; & Lake sagara (yote yakipatikana mkoa wa Kigoma)

Lake Manyara; Lake Burungi ‘ziwa sereri’; Lake Austin; Lake Balangida; Lake Tailiwi ‘Ziwa Babati’; Ambussel; Lake Kwansari (Tlawi); Lake Kimana; & Lake Basotu (All are in Manyara Region) Zaidi

Lake Jipe (Mwanga Kilimanjaro) Jipe

Lake Magadi (Simiyu-Tanzania)

Lake Mdutu au Ndutu (Arusha) SomaZaidi

Lake Magadi-(Ngorongoro-Arusha)

Lake Rukwa etc. Yaone hapa (To watch them here:)

 

Ngozi Lake 'Mbeya Region' (By: Joachim Huber-Switzerland)

LAKES NYENGINE NI: (English-Lake; Swahili: Ziwa)

  • Lake ngwazi (Iringa)
  • Lake Saosa (njombe)
  • Mkoa wa Mtwara: una maziwa ya: (Lake-Tandahimba; Mweru; Mpwapwa; Mambamba; Chidya; Kitere na Ziwa Lipelwe)
  • Mkoa wa Tanga una maziwa ya: (Lake Magoroto, na Lake Manka)
  • Pwani Regions Lakes are (Lake Tagalala; Nzerkera; Siwadu; Mzizima na Utenge; & Mansi)
  • Lake Gombo (in Morogoro Region)
  • Lake Kindai; Lake Singida; Minyere; Mikuyu; Ziwa Kitangiri; Ziwa Chaya; na Ziwa Sulunga; Yote yakipatikana mkoa wa (Singida)
  • Hombolo lake; Serya; Haubi lake & Lake Nzuhe (Dodoma)
  • Lake Ngosi / Ngozi crater (Tukuyu-Mbeya)
  • Elemeti lake (Shinyanga)
  • Liteho lake (Ruvuma)
  • Lake Momela lake in (Arusha)
  • Lake burigi (Chato-Geita) etc.

Source: 

https://traveltriangle.com/blog/lakes-in-tanzania

 

Lake Chala - Kilimanjaro (By: Joachim Huber)

MENGINE NI: ZIWA

  • Gombo, Nziwi, Haubi, Igalula, Mamka, Rutamba, Balangida
  • Lake: (Mansi, Sagara), Lelu (Sekena), Basuto (Minyere)
  • Lake Ilamba; Kingiri & Lake W.Heckmann (Mbeya-Tanzania)
  • Lake Sundu (Rukwa-Tanzania)
  • Lake: Bisongo (= Ngoma) Kajumbura, & Mkoe, (Mujunju (= Rwakajunju) Tlawi, Burungi (Kingili)
  • Ziwa Burigi; Lake Ikimba; Bisongu; Kasinga; Lwelo; Ngembe; Kaburi na Ziwa Ruko (Yote yakipatikana mkoa wa Kagera Tanzania)
  • Ziwa Welu, Empakai (Kitere)

Source: https://www.fao.org/3/t0473e/t0473e09.htm

Sunday, 30 August 2026

MJI MTAKATIFU WA JERUSALEM, MWINGILIANO, CHANZO IMANI ZA DINI TOFAUTI


Na.
Stewart Meena'

Kwa miongo kadhaa sasa, tofauti na zamani kumekuwepo na mzozo wa muda mrefu kuhusu udhibiti wa mji wa Jerusalem kati ya Waisraeli na Wapalestina, mmoja kati ya hawa akidai kumiliki eneo hilo moja kwa moja na mwingine akidai uvamizi.

Mji wa Yerusalemu (Jerusalem) umegawanywa katika pande mbili, Jerusalem Mashariki na ile ya Jerusalem Magharibi, ambapo Jerusalem ya Magharibi hutazamwa na Israel kama mji wake mkuu (tokea ilipotangaza hilo 1980 kama mji wake mkuu wa milele), huku Jerusalem Mashariki hutazamwa na Palestina kama mji wao mkuu wa taifa lao.

Eneo lote la Jerusalem, kwa kiwango kikubwa limetawaliwa na Israel tangu vita vya mwaka 1967 taifa hilo lilipojitangaza kuwa dola huru chini ya umoja wa mataifa, ambapo Tangu wakati wa vita hivyo, Israel imejengwa nyumba za walowezi wa Kiyahudi takriban 200,000 ambao huishi Jerusalem Mashariki, hatua iliyoshutumiwa na jamii ya kimataifa kama ukiukwaji wa haki ya umiliki wa mji huo.

Ingawa inakadiriwa eneo hilo huishi Wapalestina takriban 370,000, na kutambuliwa kama eneo halali la waPalestina na Mataifa mengi ya nchi za Kiarabu na zile zenye waislamu wengi duniani.

Je! ni kwa nini mji huu huzozaniwa kwa kiasi hicho na mataifa haya mawili?

Sababu kubwa ni kuwa maeneo haya, hupewa umuhimu wa pekee na imani au "Dini kubwa tatu duniani" (Ukristo, Uislamu na Uyahudi) Ambapo imani zote hizi tatu humuangazia 'Abraham/Ibrahim' kihistoria ambaye anatajwa kwenye Biblia na Koran kama mmoja wa waanzilishi au mababu wa imani ulimwenguni kote. Mfano: 'Biblia humuita kama baba wa imani'

Kwa Kiebrania, mji wa Jerusalem hufahamika kama Yerushalayim na kwa Kiarabu al-Quds. Kwa Kiswahili, jina lake halisi ni Yerusalemu, ikiwa ni miongoni mwa mji wa kale zaidi ambao upo hadi sasa duniani.

Kihistoria mji huu uliwahi kutekwa, ukabomolewa na kuharibiwa vibaya sana, kabla ya kuja kujengwa upya tena, kwa kuyarudisha na kuhifadhi yale maeneo muhimu yaliyokuwepo tokea enzi maeneo hayo.

Eneo hili, ukichimbua sehemu ya ardhi yake kwenda chini, hufichua enzi fulani katika historia yake kuonyesha eneo ilo palikuwa na mji uliopotea (Lost city), hivyo ingawa kumekuwa na ubishani au mzozano kati ya dini mbalimbali kuhusu umiliki wa eneo hilo, lakini dini zote huungana kwa pamoja kuungama na kusali katika eneo hilo kwa vipindi na misimu, kwa kuutaja ni mji takatifu.

Ndani yake kuna Mji Mkongwe, ambao una njia nyembamba, vichochoro na nyumba za kale, ikigawanyika katika pande au maeneo manne makuu, likitofautishwa na upekee wa aina ya majengo yake kuwa na muundo wa tofauti kulingana na tamaduni za wenyeji wa mitaa husika.

Moja ya maeneo hayo manne: Kuna eneo la Wakristo, Waislamu, Wayahudi na Waarmenia, na kila eneo likiwa limezungukwa au kutenganishwa na ukuta mkubwa wa mawe. kama ilivyo kwenye ukuta wa maombolezo (Wailing wall & west bank)

Wakristo wana maeneo mawili, yale madogo ya wakristo wa Kiarmenia, na ya wakristo wengineo, kukiwa kumehifadhiwa kwa vituo vya vya kale zaidi vya wakristo hao hususani utamaduni wa Waarmenia duniani, uliohifadhiwa ndani ya Kanisa la St. James na nyumba kubwa ya utawala.

Nje ya Lango la Damascus, kuna Kanisa kuu Ndani ya mtaa huo wa Wakristo, likiwa na ukumbusho wa mahifadhio ya pango au 'Kaburi lenye historia kuhusu kifo na Ufufuo wa Yesu Kristo kama masihi na muokozi wa wakristo kote duniani. Ni eneo hilo inaelezwa 'Yesu alisulubiwa hapo, katika Golgotha, au mlima wa Calvary na hapo ndipo alipofufuka.

Kanisa takatifu hilo husimamiwa kwa pamoja na kwa ushirika wa madhehebu mbalimbali ya Kikristo wakihudumu hapo, wale wa kanisa la Kiothodoksi la Ugiriki, watawawa na mapadri wa Francisca kutoka Kanisa Katoliki la Roma na wengine kutoka kanisa la Waarmenia. Pia kuna Waothodoksi kutoka Ethiopia, Coptic na Syria.

Ni eneo ambalo mamilioni ya mahujaji wa Kikristo husafiri kila mwaka kwenda kuliona kaburi wazi la Yesu na kutafuta ufunuo na kuomba katika eneo hilo.



Al Qudus: Mtaa wa Waislamu huu ndio mkubwa zaidi kati ya maeneo hayo manne na ndani yake kunapatikana madhabahu ya Dome of Rock (Kuba ya Mwamba) na Msikiti wa al-Aqsa kwenye eneo linalofahamika na Waislamu kama Haram al-Sharif, au Mahali/Hekalu Patakatifu.

Msikiti huo ndio eneo la tatu kwa utakatifu katika dini ya Kiislamu na husimamiwa na wakfu wa Kiislamu ambao hufahamika kwa Kiarabu kama Waqf, ambapo Waislamu hao huamini kwamba Mtume wao 'Muhammad' alisafiri kutoka hapo hadi Mecca usiku na aliomba pamoja na roho za manabii wengine wote katika viunga vya eneo hilo.

Hatua chache kutoka hapo kunapatikana Dome of the Rock (Kuba ya Mwamba) ambapo kuna jiwe jeusi la msingi, huko Waislamu huamini kwamba ni kutoka hapo ambapo Mtume Muhammad alipaa mbinguni. Hadi hivi wa leo Waislamu hutembelea eneo hilo takatifu kila wakati katika mwaka ku hiji, lakini kila Ijumaa wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhan, mamia ya malelfu ya Waislamu hufika kuomba kwenye msikiti huo.



Katika mtaa wa Wayahudi, kunapatikana Kotel, au Ukuta wa Magharibi ambao ni masalio ya ukuta wa nje uliozunguka eneo lote lililokuwa Hekalu Takatifu, ambapo hapo ndipo eneo takatifu zaidi katika dini ya Kiyahudi.

Wayahudi huamini kwamba hapo ndipo kulikuwa na jiwe la msingi ambapo kutoka kwake dunia iliumbwa; Kadhalika, wanaamini ni hapo ambapo Abraham alikuwa amejiandaa kumtoa kafara mwanawe Isaac.

Wayahudi wengi huamini kwamba Dome of the Rock ndipo lilipokuwa eneo takatifu zaidi ndani ya hekalu lililofahamika kama Patakatifu pa Patakatifu.

Ukuta wa Magharibi ndilo eneo la karibu zaidi ambalo Wayahudi wanaweza kufanya maombi yao, wakisimamiwa na Rabbi wa Ukuta wa Magharibi na kila mwaka hutembelewa na mamilioni ya mahujaji wa kiyahudi kutoka kila pembe ya dunia.

Hivyo: Kwa mujibu wa imani zote hizo tulizojadili na kuuchukulia kwao kwa upekee sehemu na baadhi ya mitaa ya eneo hilo, ndio maana kumekua na kuongezeka kwa mzozano wa kiimani na kiitikadi kila mmoja kutaka kudai na kutambuliwa kuwa eneo hilo ni lake, huku wengine wakifika mbali kutaka kufuta kabisa kumbukumbu na historia za imani nyingine ili kusiwepo na muingiliano huo.

Ni maeneo haya hususani nyakati za siku kuu za kidini, umati wa wageni hufurika maeneo haya kwa lengo la kutimiza moja ya nguzo zao kiimani, kama njia ya kuenzi na kuwa karibu zaidi na Mungu muweza aliyeziumba mbingu na dunia.

CHANZO:
BBC Swahili, & Blogsite washirika

Thursday, 27 August 2026

MWANAMKE: KWANINI TALAKA HAIPASWI KUWA SULUHISHO LA MGOGORO JUU YA USALITI!

 

FIKIRIA: Mwanamke, unamuacha mumeo (Mwanaume wako) kwasababu ya usaliti, alioufanya kuwa na mwanamke mwingine, (Aah!)

Mna familia pamoja, mtoto mmoja" au wawili. (Ok!)

Hivyo, ukaomba talaka na mkatalikiana kwa sababu umeumizwa sana na usaliti wake na huwezi kuuvumilia! Na baada ya mchakato wa talaka kukamilika, ukaondoka na watoto wako! (Ooh!)

Ukaanza kufanya kazi kwa bidii ili ujipatie mahitaji yako na uwalelee watoto wako mweyewe bila kuonyesha kuhitaji msaada wa baba yao na kuzimudu gharama za maisha mwenyewe. (Good)

Ili kuendana na kuongezeka gharama za maisha, unaangukia kwa mwanaume mwengine ‘Labda tajiri) Hujali chochote maana unahitaji kulipa ada za watoto kama mwanamke unayejiamini na unajitegemea unahitaji kuuthibitishia ulimwengu unajiweza mwenyewe kwa yote ndio maana ukakubali kuwa na mwanaume huyo tajiri katika penzi la siri ingawa unafahamu ni mume wa mtu. (Unajikuta umerudia kosa lilelile lililofanya nyie kutengana kwa talaka)

Hatimaye sasa na wewe umekua mchepuko kwa mume wa mtu, tena mwenye familia yake na watoto pia (side chick to cheating situation)

Ndipo unakumbuka na unaanza kufikiria kuhusu mwanamke wa pembeni aliyekua naye mumeo, na kwa nini alikua naye! “Umechelewa’ Nda yako haipo tena!

Ulichofanya, ndicho alichokifanya mwanamke uliyemfuma na mume wako, hukufikiria kuhusu maadili, na unaanza kumuelewa taratibu: Pengine alikuwa na mume wako kwasababu ya ugumu wa maisha, wingi wa majukumu, watoto aliotelekezewa wa kuwalea! Na zaidi tumbo linalohitaji chakula kila siku.

NA SASA: Kama yule tu, unatamani hata kumpigia mwanaume wa sasa uliye naye, lakini huwezi sababu unatambua yupo na mke wake na familia yake nyumbani, na wewe unalinda nafasi yako kwake maana mkewe akigundua hawezi kukimbilia kuachana zaidi wewe ndio utaachika. “Mateso yanarudia tena upya”

Hivyo amekupa masharti yake ambayo utake usitake lazima uyafuate, na unapaswa kuheshimu faragha yao kuwa sasa yupo nyumbani na familia yake na wewe utaendelea kuwa option-tu, Linapokuja swala la Kupunguza mawazo na tamaa zake.


Unafikiria tu kuhusu maumivu yako!

Unafikiria tu kuhusu faraja (Consolation) yako!

Ila walau awali ulikuwa na mume wako pekee yako’ Ndio alikusaliti lakini bado aliendelea kuwa wako!

Hatimaye unajaribu kutafuta tena kufahamu juu ya yanayoendelea kwenye maisha yake baada ya kutalikiana na kila mmoja kushika maisha yake, unang’amua sasa ame ‘move-on’, na tayari anaishi na mwanamke mwingine pengine mdogo kiumri au mrembo kukuliko wewe.

Unakaza roho, kwakua mawasiliano yake bado unayo unaamua kupigia na kumuomba miadi ya kukutana sehemu kuongea kwa kigezo cha watoto wame-mmisi wanataka aje kuwatembelea, kweli anafika na kuwaletea vizawadi watoto na kukuachia pesa kidogo ya matumizi ya watoto, lakini haitoshelezi kama ilivyokuwa zamani. (Mke mpya ameshikilia matumizi yake yote)

Mnapanga kutoka matembezi kidogo, mnakumbushiana wakati mzuri mliokuwa nao zamani na hamadi-bila kutarajia, na ngono mnashiriki! Kwa muda mchache unasahau taabu na dhiki na upweke uliokuwa nao wote!

Punde, mmemaliza kila kitu anakuaga kurudi kwa mkewe anapiga simu, ghafla unagundua sio wako tena na dhiki, taabu na upweke unarudi kama ulivyokuwa siku zote!

NDIPO: Unagundua sasa unahusiana ‘dating’ na wanaume wawili tofauti, ambapo wote wawili wamewasaliti wake zao na wewe ndio sababu!

Ghafla unaikumbuka ndoa yako, uhuru uliokuwa nao ukiwa na mume wako wa ndoa, kisha unagundua ni kama dunia nzima imekugeukia na maisha hayako sawa kwako!


Unaweza kudhani hii ni stori tu, lakini kuna wanawake wanaoiishi kiuhalisia, na ninge’ au ningalijua huja baada ya kuwa tukio lishatokea. Siungi usaliti ndoani, Lakini pia siungi vitendo vya ukatili ndoani" Mninukuu vizuri!

Mbali ya tofauti zetu, familia ni baba na mama na sio mzazi mmoja, licha ya changamoto zilizoko ndani ya familia hizo.

Asilimia kubwa ya ndoa zinawaka moto, na sio salama kwa asilimia mia, (Ni kusameheana na kuvumiliana) Tafakari chukua hatua!

#MwalimuMeena (0778291375) Kwa Maoni, au Unahitaji ushauri wa ndoa nipo hapa kukushauri!

Unaweza kusambaza elimu hii: (Share) iwafikie wengi zaidi, lakini (usi-copy na ku-paste) na kufanya kama ni chanzo cha mawazo na Sanaa yako) ukifanya hivyo nipe credit yangu katika chapisho lako. Asante!

 LINK INTO ENGLISH VERSION: ReadMore

Monday, 24 August 2026

NINI HUTOKEA, MAUMIVU TUMBO LA HEDHI KWA WANAWAKE?

Picha: JohnsHopkin Health Blog


Kuingia hedhi ni jambo la kawaida kwa kila binti/msichana aliyepevuka itoshe kusema "Ni jambo la kujivunia" kwakuwa hedhi ni kipimo sahihi cha kuwa Mwanamke ambaye siku za usoni utatarajia kuitwa mama; na ikiwa binti huioni hedhi yako inapaswa kuwaona madaktari mapema kutibu na kushughulikia tatizo hilo haswa kwa wasichana waliokatika umri wa kuvunja ungo (kupevuka)

Nini hutokea wakati wa hedhi!?: Kibiolojia hedhi hutokea baada ya kupita zile siku za urutubishaji wa yai (Ovulation circle) ambapo hii hutukia wiki ya3 kwa wanawake wengi wenye mzunguko wa siku21, 28 na 31.

Wakati huu, Yai ambalo halijarutubishwa (kwa kukutana na mwanaume) hutolewa kutoka kwenye ovari za mwanamke kwa mfumo maalimu wa mwili (kuflashi) na hapo muhusika huweza kuona uchafuuchafu wa kawaida, na damu kwa muda wa siku2, 3 au 4, huku wengine wakienda mpaka wiki moja (siku7) ambapo hii watabibu wengi huieleza kuwa sio nzuri sana kiafya, ila kikawaida inatakiwa siku4 iwe imekata.

Ni wakati huu wa hedhi: Wanawake wengi hupitia madhila mbalimbali yakiambatana na #maumivu_makali chini ya kitovu, kuumwa na kiuno na mgongo, kichefuchefu, kukosa hamu ya kula na kutapika.

Nikiwanukuu baadhi ya kina dada wanasema:

"Mimi staki kuongea maana nahesabu siku tu nianze kuhangaika daa mungu sijui sababu zake lakini kwakweli ata ukielezea akuna atakaye kuamini";

"Maumivu ya tumbo + kiuno + kichefuchefu + kutema mate kama mjamzito, eee Mungu tusaidie sisi";

LAKINI SULUHISHO AU TIBA YAKE IPOJE?
Hakuna tiba maalumu ya changamoto hii, maana wengine hutumia dawa za asili (mitishamba) na wakapona, wengine hutumia tiba-lishe wakapona, Wengine dawa za hospitali za kutuliza maumivu wakapona.

Nikiwanukuu wadau kadhaa (wanawake) wenyewe husema:
  1. "Tunywe Maji Ya Karafuu, Ikifika Siku Wala Tumbo Haliumi"
  2. "Chai ya moto yenye mchanganyiko wa tangawizi, karafuu, mdalasini, hiliki inanisaidia sana"
  3. "Ikianza tuu day one chemsha mizizi ya mkunde pori kunywa ila hii #kupata_mimba ni nje nje inasaidia na tatizo halijirudii me nshasahau hzo mambo za kuumwa tumbo baada ya kupata ujauzito na kujifungua"
  4.  "Kpindi Cha ubinti wangu nilikuwa naumwa mnoo yaani hadi home walikuwa wanajua, lakini tangu nijifungue mwanangu siumwi tena na chochote yaan"
  5. "Tumbo la P, mdogo wangu alikuwa anaumwa mpaka anazimia... Ila tulijitajidi kumchemshia #mzugwa mara nyingi tuwezavyo sa hivi anaumwa ila cyo km zamani"
Liziki Nambale anasema: "Mimi nimeponea majani ya Mbaazi" Nakama unaumwa siku nyingi inasaidia kukata hedhi kama unaumwa siku kuanzia saba kwenda mbele au hedhi isioleweka yaani kama huna tarehe maalumu chukua hayo majani matatu ya mbaazi, yaoshe utafune mabichi, na kwamanuizi kua: Mfano-nataka kuumwa siku tatu kama aya majani utaumwa ivyoivyo" Maajabu haya ya M'mbaazi.

Wengine hutumia dawa za Hospitali za kuondoa maumivu, huyu anasema: "Unaweza ukatumia piroxicam Mana ni dawa ya maumivu ila dawa nzuli na yenye nguvu ni #hyocine au ibrufen wengine wanatumia ata mifenamic acid au Vivian au hata paracetamol.

KIPI HUSHAURIWA: Wataalamu wa dawa mbalimbali, na watabibu wa afya hushauri kila tiba au dawa inaweza kuwa na side-effect (Madhara) endapo isipotumiwa kwa usahihi, au dawa kukataana na mgonjwa husika.

Mfano: kuna dawa hazishauriwi kwa wanawake ambao wanamzio wa chakula flani, dawa au harufu fulani kama ya pafyum, marashi nk.

Hivyo: kila dawa unayotaka kutumia uwaone wataalamu wakupe njia sahihi za matumizi.

ONYO: Njia yoyote utakayotumia hapa ni kwa hatari yako (risk of your own) hatutahusika kwa madhara.
🙏 Asante kwa kutufuatilia, na tafadhali Like page hii: https://www.facebook.com/stewart.meena na utu - Follow, ili kusoma na kupata habari, na makala nyinginezo za kuvutia kama hizi.

Saturday, 22 August 2026

MFAHAMU NDEGE KORONGO AINA YA MARABOU, 'THE UNDERTAKER'

 

Picha: Wikipedia

Na.

Stewart Meena

Kutana na ndege wasio na sauti au "mlio", wenye miguu mirefu na wenye kuweza kuhimili ongezeko kali la joto" ikilinganishwa na ndege wengine warukao, na hiyo ikampatia sifa ya upekee na majina mbalimbali kama: 

"Undertaker, na Marabou storks" Kiswahili wakijulikana kama ‘KORONGO MARABOU

Ndege hawa, ni waviziaji na vyakula vyao vikuu ni pamoja na mabaki ya mizoga ya wanyama tofauti, mabaki ya vyakula vitumiwavyo na wanadamu, samaki pamoja na vyakula vingine kama, mijusi, nyoka, vyura, wadudu, panya na ndege wengine wadogowadogo.

Makazi makuu ya ndege hawa ni maeneo yote karibu na mito, maziwa, milimani ndani ya miamba, na kwenye hifadhi za wanyamapori, tambarare zilizo na miti mirefu, ambapo licha ya urefu na ukubwa wao, wanaweza kuruka katika eneo kubwa la anga na kupaa umbali mrefu.

Kuruka kwao, huweza kuruka hewani umbali wa futi-13,000 (feet) toka usawa wa bahari, na inapokuja swala la mwendokasi katika jamii yao ya ndege, Korongo huwenda hawa wakawa wana kiwango kidogo cha mwendokasi huo.

UKWELI USIOUJUA KUHUSU NDEGE HAWA.

Picha: Rubega Safari

Marabou stork, ni miongoni mwa ndege wasiovutia (ugliest bird on the world) kwa kuwatazama, kwa mwonekano wao (wakiwa na Miguu mirefu, shingo ndefu na eneo kama tumbo la kuhifadhia chakula linaloning’inia karibu na shingo yao likiwa na rangi ya pinki (Eng: a pink gular sac).

Ndege korongo huyu, hutambulikana pia kama ndege muuwaji kwa muonekano wake kwa nyuma ukiwa unamtazama, wazungu wakimuita “Nature’s eyesore / the undertaker bird” na ndiye ndege jamii ya tai mwenye miguu mirefu katika jamii hiyo centimita karibu 50, huku mbawazao zikiwa na urefu wa futi11 na kuwafanya ndege hawa kuwa na upekee tofauti na ndege wengine.

Sambamba na ndege wote kuwa au kutambulikana pia kwa milio yao, ndege hawa hawana milio hiyo, ingawa huweza kuwasikia wakitoa milio Fulani inayotokana na kugongesha midomo yao au mbawa zao.

Hadi kufikia umri wa ukomavu ndege hawa, huchukua karibu miaka mine ‘4’ na kuwafanya miongoni mwa ndegw wanaokua taratibu-taratibu Zaidi ikilinganishwa na ndege wengine wanapoanguliwa kwenye mayai yao.

Korongo hawa wa marabou, hupatikana pekee yake barani Afrika (Ukiacha waliohifadhiwa katika zoo za wanyama) kwenye maeneo ya kitropiki kwenye nchi kama, Senegal, Eritrea, Ethiopia, Somalia, Tanzania, Kenya, Uganda, Namibia, Congo, Afrika ya Kusini nk.

(Unaweza kusoma pia hapa)

Kwa nchi ya Tanzania: Ndege hawa ni maarufu Zaidi kwenye ukaanda wa ziwa Victoria na Tanganyika, na huweza kuwaona Zaidi kwenye hifadhi ya taifa ya Serengeti, Manyara, Nyerere, Tarangire nk. Ambapo wenyeji wa mikoa ya Manyara, Mara, Mwanza, Geita ndege hawa huingia hadi maeneo ya masoko na mijini.

Picha: Natalie Carberi
Marabou (Korongo) ni ndege anayependa kuchangamana Zaidi na binadamu ndani ya makazi yao na hii ni kwa ajili ya urahisi wa kupata vitoweo vyao, huku wale kwenye hifadhi ya wanayama hupendelea Zaidi kuwa karibu na wanyama wawindaji kama Fisi, Chui, Duma, Simba na Mbweha ikiwa ni sehemu rahisi kwao kuvizia mawindo yao na kuyaiba. (Marabou stork are known to be scavenger bird) Kimsingi ndege hawa korongo sio wawindaji hodari, ila ni waviziaji hodari.

Wanawezaje Kuhimili Joto Kali La Uwanda Wa Savana?



Ili kupunguza ongezeko la joto na jua kali linalowatesa ndege wengi, kwa ndege Korongo ni tofauti kidogo, ambapo miili yao inauwezo wa asili wa kubadili kanijoto mwili wao kuendana na ukali wa jua au joto la maeneo waliyopo, kuficha uso wao ndani ya mabawa na kutanua mfuko wao wa pinki uliopo chini ya shingo huwawezesha kuendana na mabadiliko hayo ya joto.

Na endapo kutakua na baridi kali na wanahitaji joto, basi hutanua mabawa yao (mbawa) na hiyo huwawezesha kurudisha kwa haraka ongezeko lao hilo la joto ndani ya miili yao.

Kimazingira kwenye jamii yao, huwenda hawa ndio ndege wavivu zaidi na wasiopenda kuhangaika kutafuta vitoweo, isipokua kusimama karibu na wanaotafuta (kuwinda) na wakishapata kitoweo chao wao ndio huenda eneo hilo na kuwafurusha kwa ajili ya kuiba kitoweo hicho. Mfano: Kanda ya ziwa huiba samaki zilizovuliwa na wavuvi.

Mazaliano yao hupendelea zaidi majira ja kiangazi wakati kina cha maji maeneo mengi yakiwa yameshuka au kukauka, kwani ndio urahisi zaidi wa wao kupata vitoweo vyao kwa urahisi zaidi.

Ni msimu huu huweza kuwaona ndege hawa wakiwa karibu-karibu zaidi, na madume wakipambana kwa midomo yao ili kuwania haki ya kumiliki korogo jike kwa ajili ya mwanzo wa mazalia yao, ambapo atakayeshinda ndio kuanzia hapo ataambatana na jike husika kwa muda wote wa kujenga kiota, kurutubisha mayai, kutaga na kuyaatamia, kisha watoto watakao anguliwa kushirikiana kuwatafutia chakula kwa pamoja hadi watakapoweza kujitegemea wenyewe.

Angalia

Ndege hawa wakishaungana, huishi hivyo wawili pekee kifamilia hadi mwisho wa maisha yao, na ajabu nyingine ni kuwa hawachanganyi mwenza na ikitokea mmoja kati yao amekufa mwingine huakia hivyo hivyo na huelezwa, sababu ya upweke na yeye hachukui muda mrefu kabla ya kufa, ambapo baadhi ya tafiti husema ndege mwenza aliyesalia huweza kujinyima chakula kama njia ya yeye kufa.

Waweza pia kusoma HAPA

MWISHO: Kwa sababu ya urefu wa miguu yao, mbawa zao na midomo yao hii huwafanya kuwa na uwiano sawa wenye kupungua uzito hivyo kumuwezesha kuruka kwa urahisi zaidi wanapopaa angani, ikilinganishwa na jamii nyingine za ndege walio na urefu na uzito kama wa kwake.

Pia eneo la pinki karibu na shingo yake, hutumia hapo kama akiba ya kuhifadhi chakula chake akiwa ameshiba, kisha kula kwa wakati mwingine hususani anapokuwa ana njaa.

Tafadhali unaposasisha (Kushare taarifa hii), hakikisha unatambulisha chanzo cha taarifa hii kwa kutupa ‘credit’ Asante! StewartMeena

Wednesday, 19 August 2026

ATHARI / MADHARA YA KUKAA NA HAJA NDOGO KWA MUDA MREFU

Image by: Harbin Clinic


Utakubaliana na mimi kwamba, kitendo cha mtu kubanwa na haja ndogo siyo kitu cha hiyari kwamba sasa mtu anaamua ngoja nibanwe na mkojo, hili ni jambo la asili na ni matokeo ya vyakula, matunda au vinywaji tunavyotumia. Kwa lugha nyingine tumekuwa tukiita kuwa ni wito wa asili au nature’s call.

Yawezekana mtu akawa katika mkutano, safarini, akawa katika mitandao ya kijamii anachati au popote pale akiwa anafanya jambo fulani na kutokana na jambo hilo, mtu akaendelea kujibana na kutokwenda kuyapunguza maji-taka mwili, haya kutoka katika kibofu cha mkojo kwa kutoa kipaumbele kwa shughuli anayoifanya kuliko kusikiliza kwanza wito huu wa asili 'kuwa kibofu chake kimejaa.

Mambo haya tunayafanya sana, utasikia, mkojo umenibana kweli, ila ngoja nimalizie hii kazi halafu niende kujisaidia, hivi ndivyo watu wengi wafanyavyo kimazoea kitu ambacho hakishauriwi kitabibu na kwa afya ya mwili wako.

Kutokana na vyakula na vinywaji tunavyotumia katika milo yetu kila wakati, kibofu cha mkojo huanza kujaa mkojo, unaojitengeneza wakati vyakula vinachaguliwa (Kuchakatwa) na mwili, hivyo mkojo unapofikia karibu mililita 50 mpaka 500 mtu huyo husika huanza kuhisi hitaji la kwenda haja ndogo (kukojoa).

Kibofu cha mkojo kimezungukwa na vigunduzi asili (Receptors) vinavyopeleka taarifa katika Ubongo kuonyesha kuwa kibofu cha mkojo kimekaribia au kimejaa, baada ya taarifa hizi kufika katika ubongo, ubongo unatoa taarifa katika kibofu cha mkojo ili kiweze kushikilia mkojo huo kwa kuikaza misuli maalumu (Sphincters) mpaka hapo muda wa wewe kwenda kukojoa utakapofika.

Kibofu cha mkojo hufanya kazi kwa mfumo wa kujiendesha wenyewe yaani, automatic, kitendo cha mtu kupuuzia kwenda kukojoa husababisha Ubongo upate usumbufu wa taarifa za kujaa kwa kibofu cha mkojo na kwa kuwa Ubongo nao hutuma taarifa katika kibofu cha mkojo kusema kuwa mkojo uendelee kushikiliwa mpaka muda muafaka utakapofika, itafika kipindi uwezo wa ubongo kutoa taarifa hizi na pia uwezo wa vigunduzi asili (Receptors) vilivyoko katika kibofu cha mkojo kupoteza uwezo wake tena wa kufanya kazi hizo au uwezo kuwa mdogo.

Matokeo yake ni mtu siku kweli anahitajika kuvumilia kidogo ili afike sehemu inayostahihi kujisaidia, lakini hawezi tena na kujikuta muda mdogo tu….mtu tayari kaloanisha nguo yake.

Mpenzi msomaji, mtu kujibana na kupuuzia kwenda haja ndogo mara kwa mara husababisha uwezo wa kibofu chake cha mkojo kushindwa kujitawala upotee.

Pia kama uwezo wa neva zinazopeleka taarifa kwenye ubongo kuhusu mabadiliko/ujazo wa kibofu cha mkojo zitaharibika, basi misuli maalumu ya kubana mkojo (sphincter) itashindwa kuachia na matokeo yake mtu ataendelea kukaa na mkojo katika kibofu chake kwa muda mwingi zaidi kitu ambacho ni hatari kwa afya yake.

Endapo mkojo huu utashindwa kutoka, utatengeneza mazalia ya bakteria na kukusababishia magonjwa ya kibofu (bladder infection), kama vile U.T.I (Urinary Tract Infections), na pia huweza kusababisha magonjwa ya figo na mchafuko wa damu, (bacteremia).

Kuna hali huwa inajitokeza kwa baadhi ya watu, yawezekana alikuwa kabanwa na mkojo au alikuwa hajahisi kwenda kukojoa, ila akinywa maji au akisikia sauti ya maji yanachuluzika mfano maji yakitoka bombani, basi atahisi kwenda kukojoa.

Mpenzi msomaji, ni vyema tukawa wasikivu pale mtu unapobanwa na haja (mkojo), hii ni kwa ajili ya afya ya kibofu chako cha mkojo lakini pia ni kwa ajili ya afya yako kwa ujumla. Kama unalo tatizo, usisite kuonana na wataalamu wa afya..

Monday, 17 August 2026

ELEWA CHANZO CHA FIGO KUSHINDWA KUFANYA KAZI (KIDNEY FAILURE)

 

Picha na: Ahli Hospital

FIGO ni miongoni mwa viungo muhimu sana katika mfumo wa utendaji kazi wa mwili wa binadamu. Wiki iliyopita nilieleza jinsi kiungo hiki kinavyopata mawe na jinsi ya kujikinga na tatizo hili.

Chanzo: Global

Nashukuru wengi wamepiga siku kushukuru kwa elimu ile. Kwa kawaida, mwili wa binadamu una figo mbili zenye maumbo yanayofanana kama yale ya maharage, yakiwa yamejificha nje ya utando unaozunguka tumbo, chini kidogo ya mbavu za chini.

Kazi kuu za figo ni kuchuja vitu mbalimbali pamoja na sumu katika damu na hivyo kusaidia katika kuhifadhi na kuthibiti kiwango cha maji na madini (electrolytes) mwilini.

Katika kutekeleza hayo, figo huchuja vitu hivyo pamoja na maji yaliyo mwilini na kutengeneza mkojo, huchuja pia maji yasiyohitajika mwilini huku yakinyonya madini na kemikali muhimu kuzirudisha katika mzunguko wa damu na kutoa nje uchafu usiohitajika.

Kazi nyingine za figo ni kurekebisha na kuthibiti kiasi cha vitu mbalimbali katika damu pamoja na kiasi cha maji katika mwili, husaidia kutengeneza kiasili cha erythropoietin ambacho ni muhimu sana katika utengenezaji wa chembe nyekundu za damu, husaidia uzalishaji wa vitamini D na husaidia pia katika kuthibiti na kurekebisha shinikizo la damu mwilini (blood pressure).

Kwa kawaida damu inayozunguka mwilini hatimaye huingia kwenye figo kwa ajili ya kuchujwa, kutoa uchafu pamoja na sumu nyingine zisizohitajika mwilini.

Kitendo hiki cha utengenezaji mkojo hufanyika katika hatua kuu zifuatazo;

Hatua ya kwanza ni UCHUJAJI.

Damu kutoka nje huingia ndani ya mafigo na kupita kwenye glomeruli, lenye umbo kama chekeche/chujio ambalo limeundwa na mishipa mingi midogo ya damu iliyojizungusha pamoja.

Vitu mbali mbali, maji pamoja na sumu zilizo katika damu inayopita kwenye vimishipa hivi na kisha kuingia katika mirija mingine mikubwa kwa ajili ya uchujaji zaidi.

Mirija inayofuata huendelea kuchuja damu na kunyonya baadhi ya vitu vilivyo chujwa kimakosa kuvirudisha mwilini, mpaka kiasi sahihi cha uchafu kinachotakiwa kuchujwa kinapokuwa kimefikiwa.

Mara baada ya mkojo kutengenezwa na kutolewa kwenye figo, husafiri kuingia kwenye kibofu cha mkojo kwa kupita kwenye mirija ijulikanayo kama ureta.

Kutoka kwenye kibofu, mkojo hutolewa nje ya mwili kupitia kwenye mrija wa urethra.

Kushindwa kufanya kazi kwa figo hutokea iwapo sehemu ya figo au figo lote litapoteza uwezo wake wa kuchuja maji na uchafu kutoka katika damu na kutengeneza mkojo.

Kitendo hiki husababisha kusanyiko la uchafu pamoja na sumu kadhaa katika damu ambazo ni hatari kwa afya ya mhusika.

Figo kushindwa kufanya kazi kumeganyika katika makundi yafuatayo, Figo kushindwa kufanya kazi kwa ghafla (Acute Renal Failure (ARF), Figo kushindwa kufanya kazi kwa kiasi (Mild renal/kidney insufficiency) na tatizo sugu la figo kushindwa kufanya kazi (Chronic renal failure).

Figo kushindwa kufanya kazi kwa ghafla (Acute Renal Failure (ARF) Hii ni hali inayotokea kwa ghafla, na kudumu kwa saa chache mpaka siku chini ya 14, na kusababisha ongezeko la kiwango cha creatinine na urea katika damu.

Hali hii huwapata karibu asilimia 5 ya wagonjwa waliolazwa hospitali kwa sababu ya matatizo mbalimbali. Aidha hali hii hutokea zaidi kwa wagonjwa mahututi na wale wanaohitaji uangalizi wa kipekee, yaani waliolazwa ICU.

SABABU ZAKE

Visababishi (au aina) vya ARF vinaweza kugawanywa katika makundi makuu matatu: Matatizo yanayoathiri mtiririko wa damu kabla ya kuingia katika figo (Prerenal causes/failure), matatizo ndani ya figo lenyewe yanayozuia na kuathiri uchujaji wa damu au uzalishaji wa mkojo (Renal causes/failure), matatizo yanayoathiri mtiririko wa mkojo nje ya figo (Postrenal causes/ failure)

Matatizo yanayoathiri mtiririko wa damu kabla ya kuingia katika figo (Prerenal causes/failure) Aina hii hutokea kwa takribani asilimia 60 mpaka 70 ya ARF zote. Katika kundi hili, figo hukosa damu ya kutosha kwa ajili ya kuchuja na hatimaye hushindwa kufanya kazi yake  ipasavyo. Mambo yanayoweza kusababisha pre-renal failure ni pamoja na:

Upungufu wa maji mwili unaosababishwa na kutapika kupita kiasi, kuharisha, au kupoteza damu kupita kiasi (kwa sababu ya ajali au kuumia), kuvurugika kwa mtiririko wa damu inayoingia kwenye figo kwa sababu ya: Kushuka kwa ghafla kwa shinikizo la damu kwa sababu ya kupoteza damu nyingi wakati wa upasuaji mkubwa, kuumia au kuungua sehemu kubwa ya mwili, au maambukizi katika mfumo wa damu (sepsis) yanayoweza kufanya mishipa ya damu kutanuka na kushusha shinikizo la damu, kuziba au kusinyaa kwa mishipa inayopeleka damu kwenye figo.

Figo inaweza kufeli pia kutokana na moyo kushindwa kufanya kazi (heart failure) au shambulio la moyo (heart attack) linalosababisha kushuka kwa shinikizo la damu na ini kushindwa kufanya kazi (liver failure) kunakoweza kusababisha mabadiliko katika mfumo wa homoni zinazoathiri shinikizo la damu pamoja na mtiririko wa damu kwenda kwenye figo.

Mwanzoni kabisa mwa pre-renal failure huwa hakuna athari yoyote inayotokea kwenye figo, na mara nyingi, figo laweza kurudi katika hali yake ya kawaida iwapo chanzo cha tatizo kitagunduliwa na kushughulikiwa ipasavyo.

Mambo yanayosababisha madhara katika figo husababaisha karibu asilimia 25 mpaka 40 ya vyanzo vyote vya ARF. Visababishi vilivyo katika kundi hili hujumuisha vile vinavyoathiri uchujaji, mtiririko wa damu ndani ya figo na seli za figo zinazoshughulika na uchujaji na ufyonzaji wa chumvi na maji.

Visababishi hivyo ni pamoja na: Magonjwa katika mishipa ya damu, kuwepo kwa damu iliyoganda ndani ya mishipa ya damu inayopita katika figo, ajali/ Kuharibika kwa tishu na seli za figo, magonjwa ya mzio katika glomeruli na figo kwa ujumla (glomerulonephritis).

Magonjwa yanayoweza kusababisha hali hii ni pamoja na maambukizi (infection) ya bakteria jamii ya streptococci.

(More: Here Endelea kusoma hapa)