Wednesday, 19 August 2026

ATHARI / MADHARA YA KUKAA NA HAJA NDOGO KWA MUDA MREFU

Image by: Harbin Clinic


Utakubaliana na mimi kwamba, kitendo cha mtu kubanwa na haja ndogo siyo kitu cha hiyari kwamba sasa mtu anaamua ngoja nibanwe na mkojo, hili ni jambo la asili na ni matokeo ya vyakula, matunda au vinywaji tunavyotumia. Kwa lugha nyingine tumekuwa tukiita kuwa ni wito wa asili au nature’s call.

Yawezekana mtu akawa katika mkutano, safarini, akawa katika mitandao ya kijamii anachati au popote pale akiwa anafanya jambo fulani na kutokana na jambo hilo, mtu akaendelea kujibana na kutokwenda kuyapunguza maji-taka mwili, haya kutoka katika kibofu cha mkojo kwa kutoa kipaumbele kwa shughuli anayoifanya kuliko kusikiliza kwanza wito huu wa asili 'kuwa kibofu chake kimejaa.

Mambo haya tunayafanya sana, utasikia, mkojo umenibana kweli, ila ngoja nimalizie hii kazi halafu niende kujisaidia, hivi ndivyo watu wengi wafanyavyo kimazoea kitu ambacho hakishauriwi kitabibu na kwa afya ya mwili wako.

Kutokana na vyakula na vinywaji tunavyotumia katika milo yetu kila wakati, kibofu cha mkojo huanza kujaa mkojo, unaojitengeneza wakati vyakula vinachaguliwa (Kuchakatwa) na mwili, hivyo mkojo unapofikia karibu mililita 50 mpaka 500 mtu huyo husika huanza kuhisi hitaji la kwenda haja ndogo (kukojoa).

Kibofu cha mkojo kimezungukwa na vigunduzi asili (Receptors) vinavyopeleka taarifa katika Ubongo kuonyesha kuwa kibofu cha mkojo kimekaribia au kimejaa, baada ya taarifa hizi kufika katika ubongo, ubongo unatoa taarifa katika kibofu cha mkojo ili kiweze kushikilia mkojo huo kwa kuikaza misuli maalumu (Sphincters) mpaka hapo muda wa wewe kwenda kukojoa utakapofika.

Kibofu cha mkojo hufanya kazi kwa mfumo wa kujiendesha wenyewe yaani, automatic, kitendo cha mtu kupuuzia kwenda kukojoa husababisha Ubongo upate usumbufu wa taarifa za kujaa kwa kibofu cha mkojo na kwa kuwa Ubongo nao hutuma taarifa katika kibofu cha mkojo kusema kuwa mkojo uendelee kushikiliwa mpaka muda muafaka utakapofika, itafika kipindi uwezo wa ubongo kutoa taarifa hizi na pia uwezo wa vigunduzi asili (Receptors) vilivyoko katika kibofu cha mkojo kupoteza uwezo wake tena wa kufanya kazi hizo au uwezo kuwa mdogo.

Matokeo yake ni mtu siku kweli anahitajika kuvumilia kidogo ili afike sehemu inayostahihi kujisaidia, lakini hawezi tena na kujikuta muda mdogo tu….mtu tayari kaloanisha nguo yake.

Mpenzi msomaji, mtu kujibana na kupuuzia kwenda haja ndogo mara kwa mara husababisha uwezo wa kibofu chake cha mkojo kushindwa kujitawala upotee.

Pia kama uwezo wa neva zinazopeleka taarifa kwenye ubongo kuhusu mabadiliko/ujazo wa kibofu cha mkojo zitaharibika, basi misuli maalumu ya kubana mkojo (sphincter) itashindwa kuachia na matokeo yake mtu ataendelea kukaa na mkojo katika kibofu chake kwa muda mwingi zaidi kitu ambacho ni hatari kwa afya yake.

Endapo mkojo huu utashindwa kutoka, utatengeneza mazalia ya bakteria na kukusababishia magonjwa ya kibofu (bladder infection), kama vile U.T.I (Urinary Tract Infections), na pia huweza kusababisha magonjwa ya figo na mchafuko wa damu, (bacteremia).

Kuna hali huwa inajitokeza kwa baadhi ya watu, yawezekana alikuwa kabanwa na mkojo au alikuwa hajahisi kwenda kukojoa, ila akinywa maji au akisikia sauti ya maji yanachuluzika mfano maji yakitoka bombani, basi atahisi kwenda kukojoa.

Mpenzi msomaji, ni vyema tukawa wasikivu pale mtu unapobanwa na haja (mkojo), hii ni kwa ajili ya afya ya kibofu chako cha mkojo lakini pia ni kwa ajili ya afya yako kwa ujumla. Kama unalo tatizo, usisite kuonana na wataalamu wa afya..

Monday, 17 August 2026

ELEWA CHANZO CHA FIGO KUSHINDWA KUFANYA KAZI (KIDNEY FAILURE)

 

Picha na: Ahli Hospital

FIGO ni miongoni mwa viungo muhimu sana katika mfumo wa utendaji kazi wa mwili wa binadamu. Wiki iliyopita nilieleza jinsi kiungo hiki kinavyopata mawe na jinsi ya kujikinga na tatizo hili.

Chanzo: Global

Nashukuru wengi wamepiga siku kushukuru kwa elimu ile. Kwa kawaida, mwili wa binadamu una figo mbili zenye maumbo yanayofanana kama yale ya maharage, yakiwa yamejificha nje ya utando unaozunguka tumbo, chini kidogo ya mbavu za chini.

Kazi kuu za figo ni kuchuja vitu mbalimbali pamoja na sumu katika damu na hivyo kusaidia katika kuhifadhi na kuthibiti kiwango cha maji na madini (electrolytes) mwilini.

Katika kutekeleza hayo, figo huchuja vitu hivyo pamoja na maji yaliyo mwilini na kutengeneza mkojo, huchuja pia maji yasiyohitajika mwilini huku yakinyonya madini na kemikali muhimu kuzirudisha katika mzunguko wa damu na kutoa nje uchafu usiohitajika.

Kazi nyingine za figo ni kurekebisha na kuthibiti kiasi cha vitu mbalimbali katika damu pamoja na kiasi cha maji katika mwili, husaidia kutengeneza kiasili cha erythropoietin ambacho ni muhimu sana katika utengenezaji wa chembe nyekundu za damu, husaidia uzalishaji wa vitamini D na husaidia pia katika kuthibiti na kurekebisha shinikizo la damu mwilini (blood pressure).

Kwa kawaida damu inayozunguka mwilini hatimaye huingia kwenye figo kwa ajili ya kuchujwa, kutoa uchafu pamoja na sumu nyingine zisizohitajika mwilini.

Kitendo hiki cha utengenezaji mkojo hufanyika katika hatua kuu zifuatazo;

Hatua ya kwanza ni UCHUJAJI.

Damu kutoka nje huingia ndani ya mafigo na kupita kwenye glomeruli, lenye umbo kama chekeche/chujio ambalo limeundwa na mishipa mingi midogo ya damu iliyojizungusha pamoja.

Vitu mbali mbali, maji pamoja na sumu zilizo katika damu inayopita kwenye vimishipa hivi na kisha kuingia katika mirija mingine mikubwa kwa ajili ya uchujaji zaidi.

Mirija inayofuata huendelea kuchuja damu na kunyonya baadhi ya vitu vilivyo chujwa kimakosa kuvirudisha mwilini, mpaka kiasi sahihi cha uchafu kinachotakiwa kuchujwa kinapokuwa kimefikiwa.

Mara baada ya mkojo kutengenezwa na kutolewa kwenye figo, husafiri kuingia kwenye kibofu cha mkojo kwa kupita kwenye mirija ijulikanayo kama ureta.

Kutoka kwenye kibofu, mkojo hutolewa nje ya mwili kupitia kwenye mrija wa urethra.

Kushindwa kufanya kazi kwa figo hutokea iwapo sehemu ya figo au figo lote litapoteza uwezo wake wa kuchuja maji na uchafu kutoka katika damu na kutengeneza mkojo.

Kitendo hiki husababisha kusanyiko la uchafu pamoja na sumu kadhaa katika damu ambazo ni hatari kwa afya ya mhusika.

Figo kushindwa kufanya kazi kumeganyika katika makundi yafuatayo, Figo kushindwa kufanya kazi kwa ghafla (Acute Renal Failure (ARF), Figo kushindwa kufanya kazi kwa kiasi (Mild renal/kidney insufficiency) na tatizo sugu la figo kushindwa kufanya kazi (Chronic renal failure).

Figo kushindwa kufanya kazi kwa ghafla (Acute Renal Failure (ARF) Hii ni hali inayotokea kwa ghafla, na kudumu kwa saa chache mpaka siku chini ya 14, na kusababisha ongezeko la kiwango cha creatinine na urea katika damu.

Hali hii huwapata karibu asilimia 5 ya wagonjwa waliolazwa hospitali kwa sababu ya matatizo mbalimbali. Aidha hali hii hutokea zaidi kwa wagonjwa mahututi na wale wanaohitaji uangalizi wa kipekee, yaani waliolazwa ICU.

SABABU ZAKE

Visababishi (au aina) vya ARF vinaweza kugawanywa katika makundi makuu matatu: Matatizo yanayoathiri mtiririko wa damu kabla ya kuingia katika figo (Prerenal causes/failure), matatizo ndani ya figo lenyewe yanayozuia na kuathiri uchujaji wa damu au uzalishaji wa mkojo (Renal causes/failure), matatizo yanayoathiri mtiririko wa mkojo nje ya figo (Postrenal causes/ failure)

Matatizo yanayoathiri mtiririko wa damu kabla ya kuingia katika figo (Prerenal causes/failure) Aina hii hutokea kwa takribani asilimia 60 mpaka 70 ya ARF zote. Katika kundi hili, figo hukosa damu ya kutosha kwa ajili ya kuchuja na hatimaye hushindwa kufanya kazi yake  ipasavyo. Mambo yanayoweza kusababisha pre-renal failure ni pamoja na:

Upungufu wa maji mwili unaosababishwa na kutapika kupita kiasi, kuharisha, au kupoteza damu kupita kiasi (kwa sababu ya ajali au kuumia), kuvurugika kwa mtiririko wa damu inayoingia kwenye figo kwa sababu ya: Kushuka kwa ghafla kwa shinikizo la damu kwa sababu ya kupoteza damu nyingi wakati wa upasuaji mkubwa, kuumia au kuungua sehemu kubwa ya mwili, au maambukizi katika mfumo wa damu (sepsis) yanayoweza kufanya mishipa ya damu kutanuka na kushusha shinikizo la damu, kuziba au kusinyaa kwa mishipa inayopeleka damu kwenye figo.

Figo inaweza kufeli pia kutokana na moyo kushindwa kufanya kazi (heart failure) au shambulio la moyo (heart attack) linalosababisha kushuka kwa shinikizo la damu na ini kushindwa kufanya kazi (liver failure) kunakoweza kusababisha mabadiliko katika mfumo wa homoni zinazoathiri shinikizo la damu pamoja na mtiririko wa damu kwenda kwenye figo.

Mwanzoni kabisa mwa pre-renal failure huwa hakuna athari yoyote inayotokea kwenye figo, na mara nyingi, figo laweza kurudi katika hali yake ya kawaida iwapo chanzo cha tatizo kitagunduliwa na kushughulikiwa ipasavyo.

Mambo yanayosababisha madhara katika figo husababaisha karibu asilimia 25 mpaka 40 ya vyanzo vyote vya ARF. Visababishi vilivyo katika kundi hili hujumuisha vile vinavyoathiri uchujaji, mtiririko wa damu ndani ya figo na seli za figo zinazoshughulika na uchujaji na ufyonzaji wa chumvi na maji.

Visababishi hivyo ni pamoja na: Magonjwa katika mishipa ya damu, kuwepo kwa damu iliyoganda ndani ya mishipa ya damu inayopita katika figo, ajali/ Kuharibika kwa tishu na seli za figo, magonjwa ya mzio katika glomeruli na figo kwa ujumla (glomerulonephritis).

Magonjwa yanayoweza kusababisha hali hii ni pamoja na maambukizi (infection) ya bakteria jamii ya streptococci.

(More: Here Endelea kusoma hapa)

Wednesday, 15 February 2023

BAADHI TABIA HATARISHI ZINAZOFANYA MTU KUTOKUELEWEKA KATIKA UHUSIANO.

Image copyright: fakazanews

 Na. Stewart Meena

Mahusiano siku hizi za karibuni yamekuwa na chagamoto nyingi sana kiasi kwamba Watu wanapoingia katika mahusiano (Uchumba) inakuwa kama kila mmoja ana mashaka na mwenzi wake kuwa je ana malengo ya kufanya maisha pamoja ama yuko kwa sababu ya jambo Fulani na anapita tu baada ya muda hudai kuachana.

Kisaikolojia: Mwanamke hupenda kwanza kasha mengine hufuatia baadae, tofauti na Wanaume wao hutamani kwanza kasha kupenda huja baadae “Yaani kupenda kwao hutokea ndani ya huo uhusiano, alikotamani kwanza” na hapa ndipo bahati mbaya kwa Wanawake huwaona Wanaume zao kama hawaeleweki, lakini pengine Wanawake hawa wameshindwa kuchunguza mambo ambayo Mwanaumeze wake hupende, kasha aishi humo na baadae kueleweka na kupenda kwa Mwanaumehuja tu moja kwa moja (Automatic)

Tabia za mwanaume zinazochagizwa na kuwa na mwanamke kwa kumtamani kwanza ndio hupelekea mwanamke husika amuone mwanaumw wake ‘Haeleweki’ kasha hujikuta amefanya maamuzi ya kumuacha Mwanaume wake, na kwenda sehemu nyingine, mpaka pale atakapopata huyo anayedhani kwake anaeleweka".

Bahati mbaya ni kuwa kwa kutokufahamu kwake, tatizo halipo hapo kwa (Mwanaume wake haeleweki) ila lipo hapa kwenye kufahamu Mwanaume wake nini anapenda kutoka kwake kwenye hayo mahusiano, na ni vipi mwanamke huyo ajiweke vile ambavyo mwanaume wake anavyopenda ili kutengeneza Uhusiano imara na wenye kuzaa matunda ya ndoa na Familia.

Kimsingi: Ulishawahi kusikia Kauli Kama hizi Kwa wanawake, wakisema mwanaume Yule haeleweki, Mpenzi wake haeleweki, au hata wale walio kwenye ndoa utasikia pia wanasema Mume wake haeleweki, mchumba wake haeleweki nk.

Nachotaka kuwakumbusha Wanawake na Wanaume ni kuwa: Mwanaume hutamani kwanza kasha kupenda huja baadae; na Mwanamke hupenda kwanza kasha kutamani kuwa na huyo mwanaume huja baadae, ‘Ndio maana wahanga wakubwa wa hii KUTOKUELEWEKA’ ni wanawake zaidi ya wanaume sababu tayari wameingia sehemu kwa kupenda kwanza, na walicho kitegemea ni tofauti sana na wanaume zao walichokiwaza.

WANAWAKE WASEMAPO ‘Mwanaume haeleweki’ HUMAANISHA HAYA YAFUATAYO:

-    Mwanaume ameshindwa kumfanya ajione yupo pekeake moyoni mwake, na pia hana uhakika yeye ndio utaolewa.

-     Mwanaume kutoa mara kwa mara zisizotimilizika, Wanawake hupenda kuwajaribu wanaume zao kwenye ahadi wawapazo.

-    Mwanaume kuficha chanzo cha kipato chake kwa Mwanamke wake, na hivyo kumfanya Mwanamke wake kushindwa kujua siku Mwanaume wake akiwa na pesa ama asipokuwa na pesa, hivyo anakuwa hana uhakika na huduma atakazozipata pindi atakapoolewa.

-    Mwanaume kuficha shughuli azifanyazo, kuficha ndugu zake, marafiki zake kwa Mwanamke husika kwa kutokutaka mwanamke huyo atambulike kwao,na kumwambia sio wakati sahihi kutambulishwa, kwa kuwa bado ana hofu ya kutambulisha kasha baadae kuachwa solemba hivyo ni kama na yeye anatega-tega hivi.

-    Mwanaume anayepoteza kumbukumbu za matukio muhimu kwa mwanamke wake, hupelekea kutoeleweka na mwanamke husika hushindwa kuelewa wanathaminiwa na kupendwa ama laah. “Wanaume wanaopoteza kumbukumbu hasa zile za muhimu kama birthday zao, Ahadi wazitoazo nk, Mwanamke hufikiri Mwanaume wake hamjali.

Image: ThePrint


HIVYO: Katika mahusiano (Uhusiano) Mwanamke anahitaji kwanza ‘Life Security’ kama ‘Kuthaminiwa, Kupendwa yeye pekeake, kuhudumiwa mahitaji yake mbalimbali, Kutunzwa au kupewa kipaumbele kwanza na (Kudekezwa – Hii ipo kwa wote wawili).

WANAUME: Kadhalika, hupendelea kufanyiwa yale wawafanyiao wenza wao, na wasipofanyiwa huanza kuwa na mashaka na sehemu waliyoko na kukaa nusunusu (Kwa mashaka) na kuwaza kuachana muda mwingi sababu tunaishi kwenye Dunia ambayo kuachana imekuwa ‘Faheni’

WANAUME WASEMAPO ‘Mwanamke haeleweki’ HUMAANISHA HAYA YAFUATAYO:

-    Mwanamke kushindwa kumfanya mwanume ajione yupo pekeake kwako, na hata iweje huwezi kumsaliti kwa wengine sababu unafaa kuaminiwa na ni mwanamke unayejiweka mbali na mambo ya anasa kama Pombe, Starehe, kwenda club nk. Lazima Mwanaume wako asikuelewe sababu mazingira kama hayo kumsaliti ki tendo la dakika1 tu.

-    Mwanamke, kutamani kila jambo zuri ufanyiwe wewe tu, na wewe huna hata siku moja unayotamani kumfanyia mwanaume wako mambo hayo mazuri wewe unayotaka ufanyiwe. Mfano: Kutafutwa kwa simu, wewe ndio utafutwe tu, vijizawadi wewe ndio upewe tu, kusifia wewe ndio usifiwe tu, birthday wewe ndio ikumbukwe tu na ufanyiwe, khaa! Kwani yeye sio mja (Binadamu!?) Lazima mwanaume wako ahisi hufurahii yale ambayo anakufanyia.

-    Mwanamke kufuja fedha, yaani wewe hujui kama kuna kupunguza matumizi yasio ya lazima sana, hujui ‘kuSave’ kwa ajili ya kesho au maisha yenu ya siku zijazo, wewe kila siku ni kuitisha vitu tu vya gharama, badala ya kupika mle nyumbanikila siku unataka mitoko ya hoteli kubwakubwa-, sawa utapewa yote hayo lakini mwisho wa siku mwanaume huyo utamuona haeleweki kwako, punde akishakutumia. ‘Wanaume hupenda na hutulia kwa Wanawake wanaoifikiria kesho yao’

-    Kama ilivyo kwa Wanaume, Mwanamke kuficha kipato chake, kushindwa kumsaidia mwanaume wake hata kwa mambo madogo-madogo, lazima taa nyekundu iwake kichwani kwa Mwanaume husika “Yaani Mwanaume anaweza kukwambia hata kwa kukutega-naumwa, sina hata pesa ya kwenda kupima, na wewe kwa kujitutumua unamwambia ‘Pole utapata, badala ya kumwambia ngoja tufanye maarifa, au nna elfu5 hapa tafuta ya kuongezea, au ngoja nikuletee paracetamol utilize maumivu nk. Mwanaume lazima akuone hueleweki na mwishowe hutafuta huyo atakayeeleweka.

HIVYO: Katika mahusiano (Uhusiano) Mwanaume kamailivyo kwa Mwanamke, naye anahitaji kwanza ‘Love Security’ tofauti na Mwanamke anahitaji kwanza (Life Security), kama ‘Kuthaminiwa, Kuonyeshwa anapendwa pia, kutekelezewa huduma na mahitaji yake mbalimbali ya msingi, Kupewa kipaumbele kwanza kabla ya ndugu zako na marafiki zako, na zaidi kumsikiliza kwa yale anayotaka ufanye na yale asiyoyataka usifanye. (Wanaume hupenda sana kusikilizwa na kupewa nafasi ya kuwa kiongozi wa uhusiano wenu, na sio kupandwa kichwani n.k).

WANAWAKE: Huwaelewa wanaume wanaotimiza ahadi hasahasa ahadi ndogondogo kwani kupitia kutimiza ahadi kunamfanya akuamini na azidi kukupenda, yaani ni Bora usimuahidi jambo lolote kuliko utoe ahadi ambazo utashindwa kuzitimiza, jambo ambalo yeye analichukulia Kama Deni.

Fikiria: Unapenda mwenza wako akufanyie nini, hivyo upendavyo vivyo hivyo Mwanza wako naye hutamani wewe umfanyie hay ohayo “Na ukimfanyia atafurahia vile ambavyo wewe ufurahiavyo”

MWISHO: Wanaume wenye kufikiria kutumia mabavu, Maneno machafu, makali au Kauli za vitisho na Kuhisi mabaya kwa mwanamke wake, “Mfano, kumwambia – Unachepuka eeh, ondoka kwenu, nitakupa talaka, nitaongeza mke mwingine n.k” huwanyong’onyeza wanawake husika na kujiona hawako sehemu sahihi, sababu Wanaume wanachopaswa kufahamu ni kuwa “Wanawake huamini maneno zaidi kuliko hata matendo” yaani Kadiri unavyomtisha mwanamke wako unamtengezea mazingira ya kujihami na kujiandaa Kwa lolote ‘Kuachana, Kuchepuka nk’.

Kama ilivyo kwa Wanawake, Wanaume pia hawapendi kuishi na mtu wasiyemuelewa, kwani kila mmoja hufikiria usalama wake kwenye huo Uhusiano, hufikiria kumpata mtu sahihi wakufanya naye maisha na atakaye mthamini katika wakati wa shida na raha hadi umauti umfike mmojawapo.

Tafadhali, uchukuapo na kunakili makala tambulisha na blog hii: Saysteefeatures.blogspot.com" asante; Share Makala haya na Wengine wapate kuelimika zaidi kuboresha mahusiano yao.

Source: (Msaada wa Mitandao Washirika)

Tufuatilie Mitandao ya Kijamii:

Facebook: www.facebook.com/stewart.meena

Instagram: @ Master The Last

Saturday, 29 January 2022

ZITAMBUE SIKU MAALUMU KUPATA UJAUZITO NA SALAMA ZISIZOTUNGA MIMBA

Menstruation_Circles: Mzunguko wa kila mwezi "Siku salama na siku za hatari kwa mwanamke kuweza kupata ujauzito" Katika mzunguko wa mwezi kwa kila mwanamke, umegawanyika katika pande tatu.
1, Mzunguko mrefu wenye siku35. 2,
Mzunguko wa kawaida siku 28. 3,
Mzunguko mfupi siku25.

Mfano: MZUNGUKO WA KAWAIDA SIKU 28: Kwenye pande hizo zote3, mzunguko umegawanyika katika "Siku salama (Pichani rangi ya Zambarau); Siku za hatari (Alama ya kijani) na siku za hedhi ambazo kimsingi ni siku2 hadi7 (alama nyekundu pichani) KiBiolojia, kwenye siku zenye alama ya kijani" Hizi ni siku ambazo mwanamke akishiriki ngono bila kutumia kinga atapata ujauzito bila wasiwasi wowote labda kama ana matatizo ya uzazi ambayo huweza kupelekea, binti au mwanamke husika ashindwe kupata ujauzito licha ya kuwa katika siku hizo.

-Sababu nyingine, kama Mwanamke yu-salama basi tatizo pia huweza kuwa ni kwa mwanaume wake kuwa na tatizo la uzazi pia. Swali ni kuwa je! Utazijuaje siku hizo za hatari? Kwanza kabisa, ili ujue siku zako za hatari lazima ujue idadi ya siku za mzunguko wako kama nlivyoainisha awali, ambapo kuna mzunguko mrefu, mfupi na ule wa kawaida unaochukua siku 28 na ndio mzunguko ambao watu wengi wanao. Unajuaje mzunguko wako? Hesabu siku tangu siku ile ya kwanza uliyoona siku zako za hedhi mpaka siku moja kabla ya kuona siku zako za hedhi zinazofuata.

(Unashauriwa uchukue miezi mitatu mpaka sita ukihesabu ili uwe na uhakika kwamba mzunguko wa tarehe zako haubadilikibadiliki, na kama umeshahesabu tayari na unafahamu vyema kabla ya kusoma makala hii twende sambamba) Mfano umeanza kuona siku zako tarehe moja mwezi wa nne alafu siku zako zingine ukaziona tarehe 29 mwezi wa nne, chukua 29 toa 1 utapata 28.. maana yake wewe unamzunguko wa siku 28.

Je! siku za hatari ni zipi? Siku ya hatari ni siku ya 14 kabla ya kuona hedhi inayofuata na sio siku ya 14 baada ya kuona hedhi iliyopita na hapa ndio watu wengi wanachanganya na kupata ujauzito / mimba. Pichani:

Mfano kama mzunguko wako ni wa kawaida siku 28, chukua 28 toa 14 utapata 14, Hivyo siku yako ya hatari ni siku ya 14, lakini kwa kua mbegu ya kiume inaweza kuishi mpaka siku tano na yai la kike linaweza kuishi mpaka masaa24 ndani ya mfuko wa uzazi basi siku nne kabla na siku moja baada ya siku ya14 kwenye mzunguko wako ni hatari kushika mimba (ufafanuzi chini) Kama mzunguko wako ni mrefu labda siku 35 basi chukua 35 toa 14 utapata 21, Hivyo siku ya 21 ni hatari na zingine ni 17, 18,19,20, [21] na 22.

Kama mzunguko wako ni mfupi, mfano mzunguko wa siku 21, sasa ukichukua 21 ukatoa 14 unapata 7 yaani siku ya saba ni siku yai linashuka hivyo ni hatari kwa huyu mtu kupata ujauzito, na hivyo siku zingine za hatari kwa mtu huyu ni kuanzia siku ya 3, 4, 5, 6, [7] na8.

Kama mzunguko wako ni wa kawaida yaani siku 28 sasa chukua 28 toa 14 unapata14 yaani siku ya 14 ndio hatari zingine ni siku ya 10,11,12,13, [14], na15.

Dalili kwamba uko kwenye siku za hatari ni zipi? Kuongezeka kwa joto la mwili kidogo, kuwa na hamu ya tendo, na kupata ute-ute mweupe kutoka sehemu za siri.

MWISHO: Maelezo hayo hapo juu yanaweza kusaidia kupanga uzazi, kuchagua jinsia ya mtoto au kutafuta mtoto wa jinsia uitakayo.

Lakini pia tarehe zote nilizoweka mabano [..] ambazo ndio tarehe yai linashuka ndio za mtoto wa kiume zingine zote zilizobaki ni za watoto wa kike "xx", kwa sababu kibaolojia mbegu ya jinsi ya kiume yenye "y" hua ikichelewa kurutubishwa hufa, na sababu za kufa, huweza kufa kwa tindikali liyopo sehemu asilia ya uzazi wa mwanamke, au kukaa muda mrefu bila yai kushuka eneo la urutubishaji.

KWA MSAADA ZAIDI: Waone WATABIBU wa Afya, kwenye Vituo vya afya karibu na wewe kwa ushauri bora zaidi kwa ajili ya kupanga uzazi, kuwa na Afya bora, pamoja na maswala yote yahusuyo Afya ya Uzazi.

Subscribe hapa (MeenaTzNews ) kama bado na Share taarifa iliyokupendeza ili wengine nao wapate elimu na maarifa zaidi utakayoyapata wewe.
"AKHSANTE"

Friday, 2 July 2021

FAHAMU: FAIDA LUKUKI KIAFYA KUWEKA KITUNGUU MAJI KWENYE UNYAYO WA MIGUU

Na: StewartMeena

Wengi tunafafamu kitunguu maji, (pichani) lakini bado wengi wetu hatufahamu faida zake nyingine, ambapo pia kitunguu maji hicho huweza kuwa tiba au dawa vilevile ambayo hukupatia afya bora, kukuondolea uchovu wa mwili, kupambana na kuondoa bakteria mwili pamoja na kupandisha kinga ya mwili.

Kama, tujuavyo: ulaji wa vitunguu maji haswa vikiwa vibichi kwa kachumbari, inashauriwa sana na wataalamu wa Afya walau kutumiwa kwenye kila mlo wako wa siku itakusaidia sana katika kuuzuia mwili wako kushambuliwa na magonjwa mbalimbali kama vile, homa, mafua "flu" kifua kubana, kuondoa harufu mbaya mdomoni, kupandisha kinga ya mwili kwa kuzipa nguvu seli nyeupe na nyekundu za mwili kupambana na maradhi hayo.

HEBU LEO TUANGAZIE FAIDA NYINGINE ZA KITUNGUU HICHO ENDAPO KIKIWEKWA KWENYE UNYAYO WA MIGUU NA KUBANWA NA SOKSI KISHA KULALA NACHO USIKU MZIMA MIGUUNI: Msomaji, je! unafahamu chini ya miguu yako kuna neva (mawasiliano) "meridians" nyingi tofauti zinazopeleka mawasiliano kwenye sehemu mbalimbali kwenye kila kiungo cha mwili wako "ndani na nje ya mwili" (zaidi milango6 ya fahamu) viungo vya ndani ya mwili wako, kamavile: figo, maini, ubongo, kibofu cha mkojo, moyo nk!?
ANGALIA KUHUSU: (FootReflexology )

Ndio fahamu hilo, kwasababu chini ya unyayo wako kumefanyizwa mishipa mbalimbali ambayo hupeleka mawasiliano ya moja kwamoja kwenye viungo vya ndani ya mwili wako na nje pia, na ndio maana chini ya unyayo, inaelezwa pia na wataalamu kuwa huwenda ndipo sehemu pekee yenye hisia mchanganyiko kubwa kwa mwanadamu..endapo ikipapaswa au kuminywaminywa na inapaswa kuwekewa uangalifu na umakini mkubwa zaidi.

Mfano mdogo, ikiwa ubongo wako umechoka, unamaumivu ya kichwa "kipandauso" au una unauchovu wa mwili Fanyiwa masaji "massages" maeneo hayo ya miguu kwa kukandwakandwa na barafu au maji ya ubaridi, halafu uone, majibu utayapata kwa mwili wako kusawijika au kuwa sawa na ubongo wako kuwa-active.

Hivyo: sambamba na hayo kitunguu maji pia huweza kutumiwa kuamsha_hisia za viungo tofauti vya mwili stimulation" na kuvifanya vifanye kazi zake kwa ubora na kiwango kilichokusudiwa kiafya.. JE! HII IPOJE!?
Mfano kwa kushusha Homa: OnaHapa Kwanza: FAIDA 

Hivyo: MATUMIZI: Chukua kitunguu maji, kikate vipande mviringo kisha viweke chini ya unyayo wako, lala nacho mpaka asubuhi Majimaji yake yatakusaidia kiafya kurekebisha mfumo wa mwili wako na kupandisha kinga mwili yako kupambana na maradhi mbalimbali, lakini pia kukuondolea harufu mbaya ya miguu.

"Kwa wale wenye miguu inayotoa harufu sababu yamiguu kutoa jasho" Fanya hivyo mara1 au mbili tu kwa wiki:::: kwa msaada zaidi watafute wataalamu wa TibaLishe waulizie manufaa zaidi ya kitunguu maji katika mwili, na matumizi sahihi ni yapi.

TAHADHARI Kila chenye faida kina hasara, uangalifu unapaswa kuchukuliwa; Isipokuwa matunda, viungo au dawa-lishe hizi, hazina madhara sana kwa mtumiaji ukilinganisha na mitishamba.

Hivyo katika matumizi yake, kitunguu hiki hakipaswi kutumiwa zaidi ya mara1, na pia kikishakatwa kilichosalia kisitumiwe sababu kinaweza kutengeneza bakteria sababu ya uchachu-asidi wake.. hivyo vitunguu vizuri ni vile vilivyo-"fresh" tu.

(Kwenye makala zijazo, nitachambua, Maajabu na ni kwavipi mguu unaweza kutumiwa kuamsha hisia za kufurahia tendo ktk mahusiano) Kupata makala kama hizi, tafadhali LIKE PAGE yetu hii (History And Amazing Things) inayopatikana kwenye facebook: Kisha Share ili na wenginge wapate elimu, na maarifa uliyoyapata wewe kupitia kusoma hapa kwenye blog hii.

Monday, 24 August 2020

JE! WAIFAHAMU AFYA YAKO KUPITIA RANGI YA MKOJO (Urine Colour)?

 

Picha kwa hisani ya mtandao (Google search)

Na Stewart Meena

Je unafahamu ya kwamba rangi ya Mkojo wako (Ashakhum sio matusi nitatumia jina lake halisi badala ya kupunguza ukali wa maneno kusema  "haja ndogo" ili tuelewane) inakupa matokeo sahihi kuhusu hali ya afya yako?

Lakini pia wajua maji ndio afya yako! Kwa sababu asilimia kubwa ya ufanyizo wa mwili wako ni maji (Yaani damu+maji) na asilimia 25% ni mjumuisho mwingine kwenye mwili wako, mfn. Nyama za ndani na nje nk.

Kama jibu ni hapana basi "MAKALA HII" inakusu wewe moja kwa moja; Kwani rangi ya mkojo kwa mujibu wa watalamu wa afya kupitia mahojiano mbalimbali niliyoyafanya na madaktari na wataalamu wa tiba za asili, pamoja na tafiti zangu zingine nlizozifanya kwa kuandika, au kusoma vitabu na majarida mbalimbali yahusuyo Afya:

(Nikiwa Fani yangu ni Mwandishi wa Habari)

Nimekuja na majibu kuwa kupitia Rangi ya mkojo wako unauwezekano mkubwa na ndio kipimo sahihi kinachoweza kukupa ukweli wewe juu ya afya yako, kuweza kujua dalili za awali kabla hata ya kwenda kupima maabara au kufanyiwa uchunguzi wa vipimo na daktari.

Ndio ili daktari ajue wewe unaumwa nini, au niugonjwa gani unakusumbua kwa wakati huo "ukiacha scanning na kupigwa picha ya X-rays" Daktari huitaji kupima damu yako kwa matatizo ya nje ya mfumo wa tumbo lako au kupima haja ndogo (mkojo) na (haja kubwa) ili kujua matatizo ya ndani ya mfumo ulioko tumboni mwako.

Asilimia takribani 75% kwa 25% ya mwili wako ni maji, damu na nyenzo mwili nyingine, na vyote hivi hufanya kazi kwa pamoja katika kuendesha maisha ya muhusika na ikiwemo mwili kujitengenezea kinga yake ya kutosha na muhusika kuishi kwa afya bora.

Naposema matatizo ya ndani ya mfumo uliopo tumboni (namaanisha magonjwa ambayo tunayahisi kupitia eneo la tumbo letu) Kama vile, maumivu ya tumbo na yanayoweza kuambatana na vichomi vya mara kwa mara, ambayo haya huweza kusababishwa na maradhi-mwili kadhaa ya mfumo huo kama vile typhoid, amoeba, Vidonda vya tumbo, matatizo ya figo na ini, Safura, kansa ya utumbo, Chango na ngiri nk.

HEBU NA TUJADILI SASA UTAMBUZI WA AFYA YAKO KUPITIA RANGI YA MKOJO.

Maelezo Mengine Kwa kina:

HAPA

Picha kwa hisani ya mtandao (Google search)


Kwa kawaida mkojo tuutowao una rangi mbalimbali (pichani) zenye majina yake kufuatana na rangi au muonekanao wake, Na hiyo huchagizwa na mazoea ya mtu kuijali afya yake au kuipuuza afya yake kwa kujua au kutokujua.

(Ndio mbona uvutaji wa tumbaku au sigara na unywaji wa pombe kupita kiasi ni hatari kwa afya yako, na imeandikwa hivyo lakini bado watu wanakunywa pombe kupitiliza na kuvuta tumbaku!?).

Sawa, sasa na hebu tuanze  kuzichambua rangi hizo (Pichani) na ZINAVYOASHIRIA KWENYE AFYA YA MWILI WAKO.

No1. (Transparent)

Mweupe kabisa au Mkojo usio na Rangi ya mkojo (Light yellow): Inaashiria Unakunywa maji mengi sana, na sumu iliyoko katika mwili wako inasafishika vyema, Kwani figo yako kwa msaada wa maji mengi mwilini huchuja sumu na taka mwili vyema kwa kutenga virutubisho mwili na taka-mwili.

Kiafya, mkojo wa rangi hiyo (Nyeupe kama maji) sio mzuri sana na huweza kuwa kwenye mwili wako kuna kasoro fulani au mmeng’enyo na huenda uchakataji wa virutubisho na kuondoa sumu mwili haiko sawia kwako (balanced)

KIAFYA: Binadamu anapaswa kunywa walau glasi 8 za maji kwa siku hadi lita mbili, na sio pungufu kwa faida za kiafya, hivyo kunywa maji pia kupitiliza huleta matokeo mengine tofauti kiafya.

Hivyo unashauriwa, utakapoona mkojo wako hauna rangi ya mkojo yani unatoka mweupe kama rangi ya maji hapo Kiafya kuna jambo haliko sawa (balanced) kwa hivyo unatakiwa aidha kupunguza kidogo unywaji mwingi wa maji au kuzingatia ulaji sahihi vya virutubisho mwili (balance-diet)

No2. (Lemonade) Hiyo ni Excellent / great / better / Very good

Manjano isiyokoza (Light yellow) inaashiria  unakunywa maji ya kutosha, afya yako iko vizuri na imara, hauna matatizo yoyote hivyo endelea kufanya unacho kifanya kwa kula vyakula "balanced-diet", kula matunda na kunywa maji mara kwa mara.

KIAFYA: Wewe unashauriwa ushikilie hapo hapo katika utaratibu wako wa maisha ya kila siku "life style" kwani mwili wako unajiendesha vyema.

Ili Kupata matokeo haya: Unapaswa kula vyema vyakula vyenye virutubisho mwili vyote (Wanga+Protini+Vitamini) ikiwemo na matunda kwa kuzingatia ulaji sahihi (Balance diet) pamoja na unywaji wa maji mara kwa mara hata pasipo kuhisi kiu (isipungue glasi 6-10 kwa siku)

No3. (Light like a beer)

Majano isiyokoza (yellow) yaani rangi halisi ya mkojo, inayokaribia kufanania na rangi ya asali na isiyotoa harufu kali, inaashiria afya yako kwa wakati huo haina matatizo yoyote na unazingatia ulaji mzuri wa vyakula na unaupenda mwili wako, #Isipokuwa tatizo lako ni kuwa sio mnywaji mzuri wa maji ya kutosha vyema hivyo mwili wako hauna maji ya kutosha.

KIAFYA:

Ukiona hivyo hupaswi kuwa na wasiwasi, kwani kwa unywaji wako mdogo wa maji bado mwili wako unajitengenezea maji ya kutosha pengine kutokana na aina ya vyakula uvilavyo pia.

Isipokuwa unashauriwa tu kuongeza unywaji wa maji zaidi kwa siku kabla ya kula na baada ya kula unatakiwa usubiri angalau dakika20-30 hata kama hauna kiu ili kurahisishia figo yako ufanisi wake zaidi.

No4 (Amber) that is Bad/Warning

Manjano iliyochanganyika na uKijani kwambaali (Amber) Inaonyesha mwili wako upo upo "kawaida" na una afya ingawa si mnywaji wa maji mengi na unasubiri hadi uhisi kiu ndio unywe tena kidogo ndio maana unapokojoa mkojo hutoka na harufu kali, hauzingatii ulaji wa virutubisho-mwili sahihi (yani wewe hauli balance-diet kwa kuegemea aina ya vyakula fulani pekee na mara kwa mara, haswa vile venye rangi ya uKijani kama mbogamboga na matunda" (mwili unatengeneza vitamini na wanga pekee), ila kwa uchache unywao Mwili wako una maji ya kutosha.

KIAFYA: Ukiona hivyo ni ishara ya tahadhari au onyo mwili wako unakupatia ujumbe kuwa kuna kitu au jambo haliko sawa mwilini mwako hivyo yakupasa ubadili mfumo wako wa maisha mara moja; pia unatakiwa uzingatie unywaji wa maji hata pasipo kuhisi kiu, pamoja na kula kwa kuchanganya vyakula vyenye kuupatia mwili wako madini ya protini kwa wingi na Vitamini-C.

Protini inapatikanaje!?

Hii hupatikana kwa kula vyakula kama Nyama nyekundu (Ng'ombe, mbuzi nk) pamoja na vitu kama Maharagwe, samaki, maziwa nk.

No5 (Very bad / Worse)

Manjano iliyochanganyika na nyekundu au rangi ya udongo (Brown) isiyo na harufu kali ya mkojo na yenye harufu kali au ya wastani, Inaashiria Upo kawaida tu ila mashakani, sababu wewe kwanza si mywaji wa maji, pili hauzingatii ulaji sahihi wa chakula na pengine hauli kwa muda sahihi pia na upo hatarini kupatwa na Vidonda vya tumbo (ulcers) Tatu, kuna aina ya kemikali unazokula au kunywa na kusababisha mwili kukaushwa maji yake kwa wingi zaidi.

KIAFYA:

Kunywa maji ya kutosha kwa siku mbili au tatu, na kama hali ikiendelea hivyo yakupasa umwone daktari upesi kwa vipimo vya mkojo wako kujua kama una UTI, baikteria mwilini waletwao na unywaji wa maji machafu "typhoid" nk.

LABDA NIELEZEE HAPA KIDOGO:

Kuna aina ya vinywaji na vyakula tunavyokula ambavyo huweza kufyonza maji-mwili kwa wingi zaidi au hata kazit unazozifanya kwa kupata mkate wetu wa kila siku.

Mfano kazi za kutumia nguvu sana, kukaa karibu na moto kwa muda mrefu zaidi, kufanya kazi viwandani haswa vile vyenye kutumia nishati ya umeme au moto na makaa ya mawe nk.

Kutembea kila siku umbali mrefu tena juani kwenda na kurudi; kubeba mizigo mizito nk inafyonza sana maji mengi mwilini.

Ukiwa mpasuaji mbao kunywa maji yakutosha, ukiwa unafanya kazi ya upishi hakikisha unakunywa maji ya kutosha tena mara kwa mara, ukiwa fundi ujenzi, makenika, injinia, dereva, mbeba mizigo mizito, mfanyaji mazoezi mara kwa mara, mwana michezo, mchumia juani nk. Hakikisha chupa ya maji haibanduki pembeni yako na unakunywa maji mengi mara kwa mara.

Ndio maana wataalamu wanasema na kushauri: Ikiwa unaishi kwenye ukanda na mikoa yenye joto kali (Dar es  Salaam, Tanga, Pwani, Morogoro, Dodoma, Mara, Mwanza, Singida, Mtwara, Kilimanjaro "sehemu baadhi" nk) yakupasa unywe maji mengi kwa siku kwa sababu maeneo hayo humfanya muhusika kutokwa na jasho jingi kupita kiasi hata bila kufanya kazi nzito au kufanya mazoezi.

Kutokunywa maji hayo hupelekea mwili kudhoofu, kuharibu mfumo mzuri wa uchujaji wa sumu mwili, chakula kutokusagika na kuchaguliwa vizuri nk. Na ikidumu hivyo kwa muda mrefu ndipo mtu unaweza kupatwa na #magonjwa hatari zaidi kama vile figo kufeli, kupata vidonda vya tumbo, ini kuungua, Kinga za mwili kushambuliwa na magonjwa mengi zaidi na kwa mjumuisho wa hayo yote na pasipo kupata suluhisho la kitabibu kama kumuona Daktari kinachofuatia ni kifo tu hakuna cha ziada.

Muhimu kutambua ni kuwa: Mwili wa Binadamu hutegemea kupata maji yake kupitia pia aina ya vyakula unavyokula kila siku, matunda, vinywaji, maji yenyewe na virutubisho-dawa, ambapo kwa mjumuisho wavyo mtu huweza kuwa na maji ya kutosha mwilini, kuwa na afya njema, kinga za mwili kufanya kazi sawia, na Kupambana na maradhi nyemelezi, mwisho maradhi shambulizi yatakupitia pembeni (utayasikia kwa jirani tu)

Mwili unafanyizwa na seli mbili za damu (nyeupe na nyekundu) ambazo hizi ndio ngao zetu, kinga na ndio huyafanya maisha yetu yasonge.

Ndio maana ukipungukiwa na damu wewe ni wa ICU, ukipungukiwa na maji wewe ni wa ICU pia na uzembeaji kidogo, malaika mtoa roho utamuona akipita pembeni yako mara kwa mara.

(NDUGU ZANGU AFYA NI MALI NA NI UHAI WAKO USIUCHEZEE

Swali la kujiuliza kabla ya kuhitimisha ni kuwa: Je! Unawezaje kuchezea uhai wako na afya yako!?

Binadamu huchezea afya yake na kuhatarisha uhai wake kwa kufanya mambo mbalimbali (mengi unayafahamu) na ndio maana unaweza kumsikia mtu akisema maisha yenyewe mafupi haya!?

Sababu anafanya jambo ingawa anatambua madhara yake, na hii ni kweli kabisa watu wengi walioelimika Wasomi ndio haswa huongoza hapa: ni walevi wa pombe kali, watumiaji wa madawa ta kulevya, hawazingatii ulaji sahihi na kwa wakati hupuuzia taarifa kama hizi (uisomayo) na mwisho wa siku pyuuuuuuu! They disappear forever!

Sio ajabu kizazi chetu cha leo (karne ya 21) kumuona kijana umri mdogo kabisa lakini Kimuonekano kashaZeeka kabisa, ndio si tunawaona mtaani huko!?

Wazee wetu (miaka ya 60, 50, 40, kurudi nyuma) ukiwaona leo hii bado ni imara licha ya changamoto ya maisha na umaskini na huwezi kuwasikia wakiwa na matatizo kwa wingi kama tuliyonayo vijana wa miaka hii (80, 90, 2000 kuja mbele) ambapo magonjwa kama presha, kizukari, miguu kuvimba, utasa, kupoteza nguvu za kiume, yote haya anayo mtu mmoja..

HIYO NDIO KUCHEZA NA AFYA NA UHAI WAKO PIA.

Ndio! Ukipatwa na hayo yote mwisho wa siku unafikiri nini kinafuatia!? Saa nyingine hebu tuache kumbebesha MUNGU lawama na mizigo asiyostahili, amekupa maarifa ya kutambua mema na mabaya yatumie!?

Acha kuwa kichwa_maji (ashakhum sio matusi) Huwezi ukaambiwa unywaji wa pombe kupitiliza ni hatari kwa afya yako bado unakunywa! Tumbaku, bangi, cocaine ni hatari kwa afya yako bado unavuta!?

Kunywa maji mengi bado hunywi!, kula mlo kamili (balance diet) bado huli wakati afrika tumejaaliwa vitu vyote hivyo, ungekuwa unaishi jangwani (deserts) ungesemaje!?

Wewe si mnywaji wa maji, hivyo Endelea kunywa maji ya kutosha walau glasi 4-8 au zaidi kwa siku, ukipata #Stakafeli kula, juisi ya Miwa, ndizi, nanasi, chungwa, limao, tangawizi, karafuu, nazi, mihogo, #maharagwe, viazi "sio vya kukaanga na mafuta" kula.

Embe, limao, nyama, bamia, mboga za majani kulaaa-uwiiiiii! Hahaha! Vingine unavijua! (Muhimu hakikisha mlo wako unajumuisha virutubisho na madini ya  -  Vitamini, wanga na protini)

Makala zinazofuata, ntajaribu kukuorodheshea baadhi ya vyakula na matunda ambavyo huweza kuupatia mwili vitamini, wanga na protini.

KUMBUKA: Rangi ya mkojo inayotoka na “Uwekundu (mfano wa damu) na mkojo unaotoa harufu (Red urine colour) Ndugu yangu hapo kimbilia kituo cha Afya kilichopo karibu na wewe, na sio kuendelea kukaa nyumbani na kutumia muzugwa, dawa za miti shamba (hapo punde tunaweza kukuimbia ule wimbo wa parapanda)

RANGI HIYO KIAFYA: Mwili Upo kawaida (sababu bado unaweza kujihisi una nguvu kiafya) ingawa sumu mwili iliyopo katika damu haichujwi vyema na kusafishika na figo

zako, yaani Ini limekataa kufanya kazi yake, hivyo madhara ya hivi muda mrefu huweza kuzalisha matatizo katika figo zako kufa kabisa, kupata vichomi vya mara kwa mara, tumbo kuuma, mwili kuishiwa nguvu nk.

HEBU SOMA HAPA KUHUSU KUJUA KAMA FIGO ZAKO ZINA HITILAFU:

(Chuchuza Figo)

MKOJO wenye Rangi ya Pinki, damu ya mzee na inayokaribia kuwa kama Nyekundu

(Blood colour). Kama hujala matunda yoyote, chakula, au kinywaji chenye asili ya uwekundu kwa wingi" (juisi ya rangi, ubuyu wa rangi nk)

Au Mwanamke haupo kwenye siku zako za hedhi (ashakhum sio matusi)" basi huwenda una matatizo makubwa kwenye mwili wako, ambapo damu hulazimika kuchanganyika na njia ya mkojo "kwenye kibofu chako cha mkojo".

Ukiona dalili hiyo tambua kuwa Inaweza ikawa sio ishara mbaya kwa mara moja ila ikijirudia kwa muda wa siku zaidi ya 2 au 3 ni tatizo hilo, tena lenye kuhitaji vipimo na matibabu ya kidaktari upesi zaidi.

Muone daktari haraka sana Ufanyiwe Vipimo kujua kama, unakabiliwa na magonjwa yepi.

LABDA NIELEZEE KIDOGO HAPA:

Mara nyingi (sio zote) mkojo kutoka na rangi ya kama damu huwa inachagizwa na kuchanganyika na damu, na hadi ikitokea hivyo zaidi ya mara2 au siku2, (Isipokuwa wanawake wakati wa hedhi) basi kuna jambo ambalo halipo sawa mwilini. "Mwili una dosari fulani)

Na huwenda muhusika anakabiliwa na magonjwa kama vile ya zinaa (mf.Kaswende, pangusa nk); au kinaMama kuwa na tatizo kwenye mlango wa kizazi "mwanamke", kuathirika kwa ini, tatizo katika kibofu chako cha kuhifadhia mkojo, njia ya kupitishia mkojo, au pengine inaweza ikawa ishara ya ugojwa wa Figo, Ini au uvimbe kwenye njia hiyo ya mkojo nk.

PATA USHAURI WA KIDAKTARI NA PIMA AFYA YAKO MAABARA AU KITUO CHA AFYA AU KWA KUJICHUNGUZA MABADILIKO YAKO MARA KWA MARA MWENYEWE HUKU UKIJIPENDA NA KUILINDA AFYA YA MWILI WAKO PIA.

ENDELEA HAPA ZAIDI (Chanzo kingine):

Tafadhali waweza tufuatilia pia Facebook kwa page yetu ya: (FB-Page)

Saturday, 11 January 2020

FAHAMU VIRUTUBISHO MUHIMU KWA AFYA YA UZAZI YA MWANAUME


Asali, mbegu za maboga "binjira", Ugali wa dona, Kitunguu saumu, Tikiti maji, Chumvi ya mawe, Tangawizi, Parachichi, Maji mengi ya kunywa, Mdalasini, Viazi vilivyochemshwa na mbogamboga za majani, ni miongoni mwa virutubisho muhimu kwa afya ya Mwanaume.
Ikiwa ni mwaka 2020, na baada ya kimya kirefu kidogo hatimaye tumerudi tena kukuletea zile Makala zako pendwa katika blogi hii, nikukaribishe tena tuwe pamoja.
Makala hii ni maalumu kwa ajili ya wanandoa tu na si vinginevyo au kama elimu kwa wanandoa watarajiwa. Muogope Mungu uzinzi ni dhambi kubwa sana.
Katika kilele cha juu kabisa cha furaha katika ndoa, kama inavyojulikana, ni sherehe inayopatikana katika tendo lenyewe la ndoa, Ingawa, ili furaha hiyo ipatikane ni lazima tendo hilo liwe limefanyika katika hali ya afya kwa wanandoa wote wawili.
Nguvu za kiume ni neno linalotumika mara nyingi kumaanisha ‘Uwezo wa mwanaume kufanya tendo la ndoa’. Na inapokuwa tofauti na hivi, tunaita ni ‘kupungua au kukosa nguvu za kiume’.
Kupungukiwa kwa nguvu za kiume hutofautiana toka mtu mmoja hadi mwingine. Inaweza kuwa ni hali ya kutokuwa na uwezo wa kusimamisha maumbile hayo, au hali ya kutokuwa na uwezo wa kufika kileleni kwa muda mzuri wa kutosha.
Pamoja na hayo yote, elimu mhimu ambayo mwanaume anatakiwa kuwa nayo, ni kuwa nguvu za kiume hazipatikani kwa kutumia madawa ya kemikali au mahala pengine; bali zinatokana na vyakula tunavyokula kila siku.
VYAKULA VINAVYOONGEZA NGUVU ZA KIUME
Chukuwa punje 8 mpaka 10 za kitunguu swaumu, menya na uzikate vipande vidogo vidogo kisha meza na maji vikombe 2 kutwa mara 2 kwa mwezi mmoja.
Pia hakikisha kila chakula unachopika basi kitunguu swaumu lazima kiwemo kama moja ya viungo na ukiweke mwishoni mwishoni kwamba kisiive sana katika moto wakati unapika hicho chakula.
Kula tikiti maji kila siku huku ukitafuna na zile mbegu zake, fanya hivi siku zote.
Kula ugali wa dona kila siku. Ni mhimu kuachana na mazoea ya kula ugali wa sembe. Ugali wa dona una virutubisho vingi na mhimu kwa ajili ya afya ya mwanaume. Kama ugali wa dona unakukera jaribu kufanya hivi, chukuwa mahindi kilo10 ongeza ngano kilo3 na usage kwa pamoja, ugali wake huwa ni mlaini, mzuri na mtamu na unaweza kula na mboga yoyote tofauti na lile dona la mahindi peke yake.
FANYA HIVI KATIKA FAMILIA YAKO KWA MAISHA YAKO YOTE
Chumvi ya mawe ya baharini ile ambayo haijasafishwa au haijapita kiwandani ina mchango mkubwa sana katika kutibu tatizo hili. Tumia chumvi hii kwenye vyakula vyako kila siku.
Kunywa maji ya kutosha kila siku bila kusubiri kiu. Kila mtu anahitaji glasi 8 mpaka 10 za maji kila siku. Maji ni mhimu katika kuongeza damu, kusafisha mwili na kuondoa sumu mwilini.
Ziloweke katika maji yenye chumvi, zikaushe, Zikaange kidogo bila kuziunguza, Tafuna mbegu 100 kutwa mara 3 kwa muda wa mwezi mmoja, Ukitafuna meza vyote, hakuna cha kutemwa hapo.
Mbegu hizi sifa yake kubwa ni kuongeza wingi wa mbegu za kiume (manii), kama unatatizo la kuwa unatoa manii machache (low sperm count) basi hii ni mhimu sana kwako.
Chukuwa lita moja ya asali safi ya asili ambayo haijachakachuliwa, ongeza vijiko vikubwa 4 vya mdalasini ya unga changanya vizuri pamoja; Lamba kijiko kimoja kikubwa cha chakula kila unapoenda kulala. Fanya hivi kwa mwezi mmoja.
Tangawizi ni chakula ambacho husisimua sana mfumo wa mzunguko wa damu mwilini, na tangawizi zinajulikana sana kwa kusukuma damu kwenda sehemu za viungo vya uzazi yaani uke na uume. Inaweza kuliwa mbichi, au kupikwa au kuanikwa na kuwa kama unga.
Ulaji wa tangawizi mbichi nusu saa kabla ya tendo la ndoa husaidia katika kuongeza hamu na nguvu ya tendo la ndoa.
Unaweza ukanywa chai ya tangawizi tu nusu saa kabla ya kuanza tendo au unaweza ukatafuna kipande cha tangawizi mbichi kwa ukubwa wa dole gumba la mtu mzima nusu saa kabla ya tendo.
Kunywa chai ya tangawizi mbichi kila siku, katika chai hiyo unayopika ndani yake weka tu maji na Tangawizi mbichi uliyosagia ndani yake (usiongeze majani ya chai humo), kumbuka tangawizi inaoshwa tu na maji na uisagie ndani ya sufuria pamoja na ganda lake la nje.
Sasa badala ya kutumia sukari wewe tumia asali kwenye hii chai yako ya tangawizi na ukiitumia hivi kila siku hutachelewa kuona faida zake. Tangawizi peke yake ni dawa ya zaidi ya magonjwa 72 mwilini!
Source: FadhiliPaulBlog

Thursday, 8 November 2018

UKWELI USIOUJUA KUHUSU RADI (THUNDER STORM) NA CHANZO CHAKE (LIGHTNING)



Na Stewart Meena

Radi hutokana na mvutano wa hali ya hewa kinzani katika tabaka la juu la mawingu ambapo ukinzani huo huchagizwa na mabadiliko ya hali ya hewa, mgando wa barafu “kuganda na kuyeyuka” matone ya mvua pamoja na mwendokasi wa mzunguko wadunia “kujizungusha yenyewe kwenye mhimili wake (rotation) na kuzunguka jua (revolution) pamoja na sayari nyingine.
Kimsingi katika dunia yetu ambayo ni sayari ya3, kumegawanyika karibu matabaka 4 ya mawingu, ambapo tabaka la juu kabisa hujulikana kama (stratosphere) na eneo la kwanza la tabaka hilo, hutafsiriwa kama mwisho wa upeo wa macho yetu kwa kuangalia angani, ambapo eneo hilo sio eneo la mawangu halisi.

Eneo unapoona rangi ya bluu na nyeupe hapa ndipo mwanzo wa mzalisho wa mawingu yenye barafu katika tabaka la pili la juu yake ambalo hilo ndilo husababisha mvua kunyesha pindi barafu inapoyeyuka kwa joto kupenya eneo hilo.
Eneo hili la kwanza sio mawingu halisi isipokuwa ni msafirisho wa mvuke na ukungu (fogs) unaozalishwa kwa baridi kuendelea kuzidi kwani kwa kadiri unavyopanda juu kutoka usawa wa bahari ndipo ongezeko la baridi linapotokea kwa wale waliobahatika kupanda mlima kama Kilimanjaro ukiwa karibia kileleni ukiangalia chini huwezi kuona villivyopo chini badala yake utaona ukungu huo mweupe unaotanda eneo hilo, na hii ndio sababu maeneo yote ya uwanda wa juu kaskazini na kusini kwa Tanzania yetu kunakuwa na baridi kali muda wote wa mwaka kutokana na mwinuko wao kutoka usawa wa bahari. Mfano:Iiringa, Mbeya, Arusha, Kilimanjaro, Lushoto-Tanga nk.

Mvutano wa hewa nayozungumzia ni hewa inayopatikana eneo la chini ya tabaka la kwanza la mawingu (sehemu tuliyopo) inayoitwa ‘oxygen’ itolewayo na mimea na ile ya ‘carbon-dioxide’ tuitowayo wanadamu na wanyama wengine, na ile inayopatikana tabaka la juu la mawingu naitrojeni ‘nitrogen’ hizi huweza kuchagiza tabia tofauti ya hali ya hewa katika tabaka hilo la kati na la juu la mawingu na hata eneo tulilopo la ardhi na lile la chini kabisa ya ardhi.
Na hapo ndipo huwa chanzo cha kuzaliwa kwa nishati ya radi, uwepo wa tufani kadhaa duniani kama vile vimbunga na zile za baharini, uwepo wa tetemeko la ardhi ikisababishwa na kusafiri kwa volkaniki (volcano) chini ya ardhi n.k

TUNAPOSEMA RADI NDIO NINI, NA KWANINI HULETA MADHARA DUNIANI?

Radi (thunder) sio muungurumo, kama wengi mnavyodhani ila radi ni mwale wa kama shoti ya umeme unaotokea kabla ya muungurumo na baada ya muungurumo kupita; mwale huo ni nguvu kama nishati ya umeme ambao huu huwa na vipimo-nishati zaidi ya umeme (voltage & watts) ambayo hii huwa na kiasi cha Vol. zaidi ya elfu-10 ukilinganisha na ile ya umeme inayoanzia (vol.110/220-1000)
Kama tulivyoona mwanzo kwanini radi hutukia, lakini bado watu huwa na maswali mengi kwanini mara kadhaa imekuwa ikileta madhara kwa kupiga miti’ nyumba na watu wakati mwingine, hivyo kuhusisha radi hiyo na imani za kishirikina pamoja na kuvaa aina ya mavazi.

KUNA UHUSIANO GANI:
Kitaalamu hakuna uhusiano wa radi na imani za kishirikina isipokuwa kuna mazingira yanayoweza kuifanya radi kupenya kwenye mawingu na kushuka moja kwa moja aridhini na kuleta madhara mahala ilipofikia (gravitation area).
Radi huambatana na mvua na mvutano wa nishati kama ya msumaku, na endapo ikitokea ikawa inasafiri angani na kukawa kunauvutano wowote wa mfumo wa nishati kama ya umeme, umande umande wa barafu na mazingira ya mvua huweza kupiga na kushuka hadi eneo hilo.


Ndio maana nyumba zenye umeme huekewa chuma flani ya rangi ya shaba na kuchimbiwa ardhini ili kuzuia radi hiyo kuwa na uwezekeno mkubwa wa kuipiga nyumba hiyo, na hivyo ni hatari zaidi kutumia umeme wa moja kwa moja pasipo kuweka kizuizi hicho kwasababu nishati ya radi huwa ni mara maelfu zaidi ya umeme wa kawaida

Na inapotokea radi hiyo kupiga basi tambua kuna mvutano uliopo katika eneo hilo, mvutano ambao huivuta nishati ya radi na kuileta hadi aridhini na kisha kuleta madhara kwenye eneo husika palipo na kani mvutano huo (gravitation).


Kuna uhusiano mkubwa sana uliopo kati ya nishati umeme wa radi na umeme wa majumbani, Uvutano wa sumaku, mvukizo wa joto la ardhi haswa maji yanaponyweshwa juu yake; na uwepo maji haswa yale ya mvua pamoja na yale ya bomba na aina ya nyenzo yanayopitia (mipira au chuma) wakati radi ikipiga.
Mabomba yaliyotengenezwa kwa chuma cha zinki, aluminium na shaba, hupitisha umeme na hivyo kwa kuwa maji hupita ndani yake, na ukayatumia wakati radi ikipiga kuna uhatarisho; lakini yale yaliyotengenezwa kwa mipira huwezi kuwepo kwenye uhatarishi ukilinganisha na hizo nlizozitaja.

MAVAZI:
Kuhusu mavazi hakuna uhusiano wa moja kwa moja wa kupigwa na radi na aina ya mavazi tunayoyavaa (Mfano watu husema ukivaa mavazi mekundu ni rahisi zaidi kupigwa na radi kweli?) Jibu ni kuwa sio kweli.!

Isipokuwa mavazi tunayoyavaa na tabia ya hali ya hewa kwa wakati huo, kwa kushirikiana huweza kuleta uwezekano huo kwa kufuata tabia ya miale ya radi inavyosafiri pekee na eneo ulilopo wakati huo kama ilivyo kwa tabia za vyanzo vya nishati nyingine kama jua na moto.
  • Mfano kivizikia (Physics): Jua hutufikia kwa njia a mnururisho;

  • Umeme au moto husafiri kwa njia ya mpitisho;
Hivyo katika mavazi nayo huwa na tabia yake katika kuakisi na kuvuta miale hiyo ya nguvu za sumaku, nishati ya jua, moto na nguvu nyingine za nishati ya umeme kama ilivyo kwa radi.

Mfano: mavazi meusi husharabu moto, joto au nishati ya jua;
Maazi meupe huakisi hali hiyo apo juu.

Mavazi mengine kama ‘Mekundu, Njano, Zambarau nk’ hayaakisi wala kusharabu nguvu hizo za nishati isipokuwa haya huwa na uwezo wa kutunza joto hilo kwa muda flani, na ndio maana katika uvutano wa sumaku mavazi haya na yale yenye asili ya unailoni au mipira huweza kuzalisha miale mfano wa cheche za moto ambazo hizi hutoa muangaza.
(Fanya zoezi moja: Chukua moja ya mavazi hayo, kasha yavae mwilini au yasugulie kwenye nywele zao kisha yafikiche yenyewe kwa yenyewe gizani usiku utaona yakitoa miale hiyo mfano wa cheche)

NINI KINATOKEA HAPO MTU KUPIGWA NA RADI NA UNAWEZA KUJIKINGAJE!:

Kwa utangulizi nilioueleza katika tafiti na makala yangu hapo juu: Imeelezwa kitaalamu kuwa radi huambatana na nishati nyingine duniani, na kuna uhusiano mkubwa sana kati yake na mvua/maji; uvutano wa sumaku na hali-joto ya mahali haswa ardhi wakati radi inapiga pamoja na mwingiliano wa hewa tofauti inayochagizwa na kujizungusha kwa dunia katika mhimili wake (Rotation) na kulizunguka jua (Revolution).
KUJIEPUSHA: usipende kukaa chini ya miti wakati mvua inanyesha na huku ukiwa umevaa mavazi yoyote yenye uwezo wa kutengeneza Usumaku yanapogusana (rejea kwenye mavazi juu); kuweka kizua radi majumbani unapofunga umeme lakini usipende kusikiliza redio au kutumia internet ukiwa kwenye eneo la mwinuko na penye umande umande au chini ya miti wakati mvua ninanyesha.

Unashauriwa kuepuka kutumia maji kwenye mabomba yasiyo ya mpira wakati radi inasafiri, kuoga wakati huo nk; lakini pia ni vyema ukapunguza matumizi makubwa ya vifaa vinavyotumia umeme wakati huo kama vile kuwasha Tvs, Radio, kutumia pasi na Heater kupikia au kuchemshia maji kuchaji simu kwa wakati mmoja.
MWISHO: radi ni mwale ule unaoonekana kabla ya muungurumo kusikika, na muungurumo huo huzalishwa kutokana na nguvu za radi hiyo (mwale) na mgandamizo wa barafu (Mawingu mazito yaliyoganda na matone ya mvua kugusa eneo hilo kutoka tabaka la juu zaidi la mawingu) msuguano wa hali za hewa kinzani.

Tahadhari: Radi ni kama ilivyo kwa nishati ya umeme, na huweza kuleta maafa kwa kuwakisha moto au kumuunguza muhusika, usikae karibu na nyaya za umeme (haswa unaosafirisha voltage kubwa) wakati mvua zinanyesha au radi kupiga.
JIFUNZE ZAIDI NAMNA GANI EATH-QUAKE NA THUNDER STORM’ HUTOKEA KWA KUBOFYA VISAIDIZI HAPA CHINI NA VILIVYO NA RANGI BLUU JUU:

Radi

Tetemeko la Ardhi